• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Wananchi Nsimbo punde kuhudumiwa katika Hospitali ya Wilaya.

Imewekwa: January 6th, 2021

Pichani:Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh.Juma Zuberi Homera( Mbele katikati) akiwa katika ukaguzi wa Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Nsimbo ulioko katika hatua za mwisho kukamilika katika eneo la Isinde Kata ya Mtapenda  Mji mdogo Nsimbo .Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mohamed Ramadhani

Na: John .A. Mganga

Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wametakiwa kujiandaa kuanza kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya inayoendelea kujengwa ambayo ujenzi wake uko katika hatua za mwisho na za kuridhisha.

Katika Ziara yake Mkuu wa Mkoa wa Katavi Juma Zuberi Homera Januari 05, 2021 aliyoifanya kwa lengo la kukagua hatua ulikofikia Ujenzi wa Hospitali hiyo ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kwa hatua ulikofikia Ujenzi wa miundombinu ya Hospitali hiyo ambapo amewataka Wananchi kujiandaa kuhudumiwa na Hospitali hiyo.

Usimamizi makini wa Mradi chini ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo  Bw.Mohamed Ramadhani pamoja na Wataalamu wengine wanaohusika katika usimamizi wa mradi huo,Ujenzi unaozingatia ubora na viwango, nidhamu pamoja na  na  matumizi sahihi ya Fedha  za Serikali ni miongoni mwa mambo yaliyomfurahisha zaidi Mh.Homera katika Ziara yake hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mohamed Ramadhani katika taarifa yake, amemuambia Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh. Juma Zuberi Homera kuwa, Halmashauri imepokea Kiasi cha Shilingi Mil.500 kwa ajili ya Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ambapo mpaka sasa Ujenzi uko katika hatua za Mwisho kukamilika.

Mkurugenzi Mohamed amesema Ujenzi wa Miundombinu ya Majengo ya Hospitali hiyo ya Wilaya uliathiriwa na changamoto ya Msimu wa Masika jambo lililopelekea kupungua kwa kasi ya Ujenzi lakini hata hivyo ujenzi huo umeendelea na uko katika hatua nzuri na za kuridhisha.

Akizungumzia kuhusu matumizi ya Fedha Mkurugenzi Mohamed amesema mpaka sasa Kiasi ha Shilingi Milioni Mia Nne Hamsini na Saba,Laki  tano sabini na nane Elfu Mia moja arobaini na tatu  ( 457,578,143) kimetumika katika Ujenzi huo kati ya Milioni 500 zilizopokelewa kutoka Serikali kuu,ambapo kiasi cha Shilingi Milioni Thelathini na nne Laki nane Hamsini na tatu Elfu na Shilingi mia moja thelathini na sita(34,853,136) zilizobaki zinatarajia kupelekwa kwa jili ya Ununuzi wa Madirisha ya Alluminium.

Aidha Mkurugenzi Mohamed amesema mpaka sasa kwa upande wa Malighafi tayari Halmashauri imekwisha nunua zaidi ya Mifuko Mia sita 600 ya Saruji kwa ajili ya kuwekea Marumaru, kwa majengo yote matatu,Marumaru zote zimekwisha fika,Uwekaji wa kiambo umeme ambapo kazi iliyobakia ni kuweka Skiming,rangi pamoja na Marumaru.

Mkurugenzi Mohamed amewahakikishia Wananchi wa Nsimbo kuwa Ujenzi wa Hospitali hiyo utakamilika ndani ya muda mfupi ujao na punde Wananchi wataepuka changamoto ya kutembea umbali mrefu zaidi ya Kilomita 16 kwenda kupata huduma katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda.




Matangazo

  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUANZA KIDATO CHA KWANZA MWAKA 2021 KUTOKA NSIMBO-DC December 19, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOPENDEKEZWA KUJIUNGA MAFUNZO YA UFUNDI STADI CHUO CHA VETA MPANDA NA CHUO CHA MAENDELEO YA WANANCHI MSANGINYA MWAKA 2021 December 20, 2020
  • KATAZO LA MIFUKO YA PLASTIKI May 20, 2019
  • ACHANA NA MIFUKO YA PLASTIKI May 20, 2019
  • Angalia zote

Habari mpya

  • Wananchi Nsimbo punde kuhudumiwa katika Hospitali ya Wilaya.

    January 06, 2021
  • RC Katavi aipongeza Nsimbo kwa Usimamizi mzuri wa Miradi

    January 05, 2021
  • Madiwani Nsimbo wahimizwa kuhamasisha Wananchi kujiunga na CHF iliyoboreshwa.

    December 23, 2020
  • Naibu Waziri TAMISEMI aipongeza Nsimbo kwa harakati za Ujenzi wa Sekondari.

    December 15, 2020
  • Angalia zote

Video

Mwenyekiti Nsimbo akemea Uchangiaji holela wa vyombo vya kunywea pombe vilabuni
Video zaidi

Quick Links

  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa
  • Orodha ya waheshimiwa madiwani
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Video mbalimbali
  • Muundo wa Halmashauri
  • Picha mbalimbali
  • Fomu mbalimbali

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : +2552955164

    Simu: +255713992124

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa