• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Baraza la Wafanyakazi Nsimbo labariki Bajeti ya zaidi ya Bilioni 20 mwaka mpya wa Fedha 2022/2023.

Imewekwa: January 19th, 2022

Pichani:Mkuu wa Idara ya Mipango Takwimu na Ufuatiliaji Bi.Victoria Cilewa akiwasilisha mbele ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi(Hawako pichani) Rasimu ya Bajeti ya Mwaka mpya wa Fedha 2022/2023 katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri.

Na: John  Mganga-DIO

Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo limepitisha makadirio ya Bajeti ya Halmashauri ya Shilingi 20,095,372850.00 kwa Mwaka ujao wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya kutekeleza programu mbalimbali zilizopangwa katika ngazi ya Halmashauri.

Mkuu wa Idara ya Mipango Takwimu na Ufuatiliaji Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bi.Victoria Cilewa Akiwasilisha Rasimu ya Bajeti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kwa Mwaka mpya wa Fedha 2022/2023 amewaambia Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri kuwa makadirio hayo ni sawa na ongezeko la Asilimia 0.98 yakilinganishwa na Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2021/2022 ambayo ilikuwa Shilingi 20,668,252,869.00

Ameeleza kuwa kati ya kiasi hicho cha Fedha,Shilingi  10,106,187,000.00 ni kwa ajili ya Mishahara,Shilingi 2,071,685,000.00  ni kwa ajili ya matumzi mengineyo ambapo Shilingi 7,917,500,850,00 imeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo.

Katika rasimu hiyo ya Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2022/2023 imeelezwa kuwa Halmashauri inatarajia kukusanya jumla ya Shilingi 1,327,189,000.00 ambapo Shilingi 1,021,980,000.00 ni vyanzo visivyolindwa(Ownsource Proper) na Shilingi 305,209,000.00 ni kutokana na vyanzo lindwa.-Bima ya Afya,NHIF,Mfuko wa Afya ya Jamii CHF pamoja na User Fee.

Aidha katika Bajeti hiyo ya  Shilingi 1,021,980,000.00 cha mapato ya ndani  kilichoidhinishwa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 Asilimia 40 sawa na Shilingi 408,792,000.00  itatumika kwa ajili ya miradi mbalimbali  ya maendeleo ambapo Shilingi 613,188,000.00 sawa na Asilimia 60 imegawanya kwenye Idara kwa ajili ya matumizi ya kawaida.

Wajumbe wa Baraza la Wafanya kazi wote kwa pamoja wameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kwa kufanikisha maandalizi ya rasimu hiyo ya Bajeti.


MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA

 

Picha 1:Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mohamed Ramadhani akifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi kilichoketi kujadili Rasimu ya Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Picha 2:Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ambae ni muwakilishi wa Vijana kutoka Chama cha Walimu Tanzania CWT Nsimbo Mwalimu Felix Ferdinand akitoa mchango wake wakati wa kujadili Rasimu ya Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2022/2023.

Picha 3;Shukuru Mukaruka Mjumbe wa Baraza la Wafnyakazi ambae ni Mjumbe wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Mkoa akichangia mada baada ya Rasimu kuasilishwa.


Picha 4;Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wakisikiliza Rasimu ya Bajeti ya Mwaka Ujao wa Fedha 2022/2023 ilipowasilishwa na Afisa Mipango Takwimu na Ufuatiliaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa