• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

BEVAC NSIMBO NA TANGANYIKA YAKABIDHIWA VITUO VYA KUKUSANYIA MAZAO YA NYUKI

Imewekwa: August 19th, 2025

Vyama vya Ushririka vya Ufugaji Nyuki katika Halmashauri za Wilaya ya Tanganyika na Nsimbo Mkoani Katavi leo vimekabidhiwa vituo vya kukusanyia mazao ya Nyuki katika Hamashauri hizo.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mheshimiwa Mwanamvua Mrindoko, Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mheshimiwa Onesmo Buswelu amehimiza wananchi na wadau wote kuendelea kutimiza wajibu wa kutunza mazingira ili kuepukana na changamoto zinazojitokeza katika ufugaji wa nyuki.

Mheshimiwa Buswelu amesisitiza wadau na watendaji wa chama cha ushirika cha ufugaji Nyuki katika Halmashauri hizo kuzitumia na kutunza vitendea kazi Pamoja na rasilimali zote walizokabidhiwa ili viweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu kwa maendeleo ya vyama hivyo katika Halmashauri zao.  “Ni jukumu langu kuwahimiza kusimamia kikamilifu uendeshaji wa vituo hivi ili vipate kudumu kwa muda mrefu, vikatekeleze mpango wa kibiashara, mpango wa kiuchumi, mpango wa kimkakakti wa kumkwamua mtanzania…………..” Ameongeza Mheshimwa Buswelu

 Mkuu huyo wa Wilaya ya Tanganyika amesisitiza kuwa ni lazima kila mwanachama kuwajibika katika kuongeza mnyororo wa kuongeza thamani ya mazao ya nyuki hasa asali ili kuboresha mazao hayo na hatimaye kupata soko la uhakika katika masoko mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.

Katika hatua nyingine, Mheshimwa Buswelu amewahimiza watendaji wote wa BEVAC pamoja na viongozi wengine kushirikiana katika utafutaji wa masoko ya mazao ya nyuki kwa namna tofauti pamoja na matangazo mbalimbali na mitandao ya kijamii ili mazao yatakayokusanywa yapate masoko ndani na nje ya nchi. “Simamieni, shirikianeni kutafuta masoko, tusije tukakusanya asali hapa tukakosa masoko, dunia sasa hivi imebadilika, tumieni kila aina ya matangazo kama mitandao ya kijamii, mikusanyiko mbalimbali kufikisha taarifa zenu za mazao ambayo mtakusanya hapa……….” Ameongeza DC Buswelu

Mheshimiwa Onesmo Buswelu amewahimiza Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri za Wilaya za Tanganyika na Nsimbo pamoja na Maafisa kutoka vitengo tofauti kuendelea kuwapa mafunzo na semina zitakazowasaidia watendaji wa BEVAC kuendelea kuimarika katika uzalishaji wa mazao yatokanayo na nyuki.

Awali akitoa taarifa ya Mradi huo, Meneja wa BEVAC Nchini Tanzania Bwana Stephen Paul amesema katika Mkoa wa Katavi, Mradi wa BEVAC unatekelezwa katika Halmashauri ya Nsimbo, Tanganyika na Mlele ambapo unatekeleza miradi mbalimbali ikiwepo kuanzisha hifadhi za nyuki kwenye misitu katika vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika na Nsimbo, kuanzishwa kwa Mashamnba darasa katika Halmashauri ili kurahisisha mafunzi kwa vitendo kwa watendaji wa BEVAC.

Bwana Stephen amesema kuwa BEVAC imefanikiwa kutoa mafunzo kwa makundi mbalimbali kama mafunzi cherehani, seremala na kuwaunganisha wafugaji wa nyuki ili kurahisisha utekelezaji wa mradi huo


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BEVAC NSIMBO NA TANGANYIKA YAKABIDHIWA VITUO VYA KUKUSANYIA MAZAO YA NYUKI

    August 19, 2025
  • BEVAC YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA CHAMA CHA USHIRIKA CHA UFUGAJI NYUKI – NSIMBO

    August 13, 2025
  • CRDB BANK YATOA MSAADA WA VITI NA MEZA SITINI KWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • NSIMBO YAPOKEA SHILINGI BILIONI 1.01 KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO KATIKA BAJETI YA 2025/2026 KUTOKA SERIKALI KUU

    August 05, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa