• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

BEVAC YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA CHAMA CHA USHIRIKA CHA UFUGAJI NYUKI – NSIMBO

Imewekwa: August 13th, 2025

Taasisi ya Enabel kupitia mradi wa kuongeza mnyonyoro wa thamani wa ufugaji nyuki yaani Beekeeping Value Chain Support (BEVAC) limekabidhi Vifaa mbalimbali vya TEHAMA kwa Chama cha Ushirika cha Ufugaji Nyuki katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani katavi.

Akikabidhi Vifaa hivyo vya TEHAMA leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bi. Christina Daniel Bunini kwa Mwenyekiti wa Chama hicho cha Ushirika cha ufugaji Nyuki wilayani Nsimbo Bwana Said Mkopi pamoja na wajumbe wengine, Bi. Christina Bunini amewataka wanachama hao kuvitumia vifaa hivyo kwa usahihi na kuvitunza katika hali ya usalama wakati wote ili viweze kuwasaidia katika majukumu yao ya kila siku na kuboresha huduma zao kwa jamii.

Bi. Bunini ametumia wasaa huo kuwapongeza wanachama wote kwa kazi nzuri inayofanywa na wanachama kupitia mradi wa BEVAC  na kuwatakia majukumu mema watendaji wote wa chama hicho hasa jukumu la kuboresha shughuli za chama hicho cha Ushirika cha Ufugaji Nyuki katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo.

Aidha, kwaniaba ya wanachama wote, mwenyekiti wa chama hicho cha Ushirika cha Ufugaji Nyuki katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bwana Said Mkopi amewashukuru wadau wote na kuhaidi ushirikiano mkubwa hasa katika shighuli za kuongeza uzalishaji wa mazao yatokanayo na nyuki.

Kwa upande wake, Afisa Nyuki katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bwana Said Mpumbi amesema Vifaa hivyo vya TEHAMA vitawasaidia kuboresha utendaji kazi wa wanachama  katika mazingira yao ya kazi, jambo litakalorahisisha utatuzi wa changamoto zitakazojitokeza kwa kushirikiana na wadau mbalimbali.

Vifaa vilivyokabidhiwa leo ni Pamoja na Printa 1, Kompyuta (Desktop) 1 pamoja na Vipima unyevu ( reflactometer)  2. Vifaa vingine vilipokelewa na Chama hicho ni Pamoja Ndoo za lita 20 zipatazo 100, bomba za moshi (bee smoker) 10, brashi za nyuki (bee brush) 30 na bango 1.

Pichani ni Wanachama wa chama cha Ushirika cha ufugaji Nyuki wakipokea Vifaa vya TEHAMA kutoka Taasisi ya Enabel kupitia mradi wa kuongeza mnyonyoro wa thamani wa ufugaji nyuki yaani Beekeeping Value Chain Support (BEVAC)

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BEVAC YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA CHAMA CHA USHIRIKA CHA UFUGAJI NYUKI – NSIMBO

    August 13, 2025
  • CRDB BANK YATOA MSAADA WA VITI NA MEZA SITINI KWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • NSIMBO YAPOKEA SHILINGI BILIONI 1.01 KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO KATIKA BAJETI YA 2025/2026 KUTOKA SERIKALI KUU

    August 05, 2025
  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPEWA MAFUNZO - JIMBO LA NSIMB0

    August 04, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa