• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

CRDB BANK YATOA MSAADA WA VITI NA MEZA SITINI KWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KATAVI

Imewekwa: August 12th, 2025

Bank ya CRDB Mkoani Katavi imetoa viti na meza sitini(60) kwa Shule ya Sekondari ya Wasichana Katavi iliyoko Wilayani Nsimbo Mkoani Katavi kwa lengo la kusaidia mkakati wa kukabiliana na upungufu wa samani katika shule hiyo, ikiwa mpango wa Benki hiyo kurudisha fadhila kwa jamii kutokana na faida inayopatikana katika miradi mbalimbali inayotekelezwa na benki hiyo.

Akikabidhi samani hizo kwa Jumuiya ya Shule ya Sekondari ya Wasichana Katavi, Meneja wa Benki ya CRDB kanda ya Nyanda za Juu Kusini Bi. Jenifer Tondi amesema kuwa Benki hiyo kupitia mkakati wake wa “Keti Ujifunze” itaendelea kushirikiana na serikali kuhudumia wananchi. Bi. Tondi ameongeza kuwa Pamoja na shughuli zake za kibenki, Benki hiyo inatenga asilimia moja ya faida yake ili kusaidia huduma mbalimbali katika jamii ikwemo afya, elimu na mazingira.

Akipokea Samani hizo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mhemshimwa Jamila Yusuph ameishukuru Benki ya CRDB kwa jitihada zake za kuunga juhudi za maendeleo katika Mkoa wa Katavi na kuwaomba wadau wa maendeleo pamoja na wawekezaji wengine kujitokeza kuisaidia jamii kwa kadiri wanavyoapata katika kazi zao. Amesema kuwa serikali inafarijika sana hasa pale wadau wa maendeleo wanapojitokeza kuisaidia jamii.

Mheshimiwa Jamila Yusuph ametumia wasaa huo kuikumbusha jumuiya nzima ya shule hiyo kuzitunza miundombinu yote ya shule hiyo ikiwa ni Pamoja na samani walizokabidiwa ili ziweze kudumu na kutumiwa na vizazi vijavyo. Pamoja na hayo, Mkuu huyo wa Wilaya ameusihi uongozi wa shule hiyo kuimarisha ulinzi katika mazingira yote ya shule ili waishio wawe salama Pamoja na miundombinu yote iliyomo.

Katika hatua nyingine, mkuu huyo wa Wilaya ya Mpanda Mheshimiwa Jamila Yusuph amewasihi walimu kuendelea kuwalea Watoto katika njia iliyo sahihi ili waweze kuyafikia malengo yao bila vikwazo. “Tunatambua sasa hivi zipo changamoto ya malezi hasa kwa Watoto wetu wanapotokea maeneo tofautitofauti, madam mmekebidhiwa jukumu hilo wanapokuwa shuleni mtusaidie kuwalea, kuwarekebisha lakini pia kuwasaidia waweze kufikia ndoto zao ……….”

Awali akitoa taarifa ya shule hiyo ya sekondari ya Wasichana Katavi, Mkuu wa Shule hiyo Bi. Elinesi Sossy Mwangomba aliainisha kuwa shule hiyo ina ufinyu wa ardhi hivyo kukosekana kwa viwanja vya michezo jambo linakosesha wanafunzi fursa ya kufanya michezo mbalimbali. Akijibu baadhi ya changamoto zilizoainishwa katika taarifa hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mheshiwa Jamila Yusuph ameahidi kushughulikia upatikanaji na uandaaji wa viwanja vya michezo ambavyo vitakuwa tayari kabla ya mwisho wa mwezi wa tisa mwaka huu.

Meneja wa Benki ya CRDB kanda ya Nyanda za Juu Kusini Bi. Jenifer Tondi (kushoto)  akiwa na wanafunzi pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mheshiwa Jamila Yusuph (Kulia) wakati wa kukabidhi viti na meza 60.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BEVAC YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA CHAMA CHA USHIRIKA CHA UFUGAJI NYUKI – NSIMBO

    August 13, 2025
  • CRDB BANK YATOA MSAADA WA VITI NA MEZA SITINI KWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • NSIMBO YAPOKEA SHILINGI BILIONI 1.01 KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO KATIKA BAJETI YA 2025/2026 KUTOKA SERIKALI KUU

    August 05, 2025
  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPEWA MAFUNZO - JIMBO LA NSIMB0

    August 04, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa