• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

HUDUMA ZA AFYA, LISHE NA USTAWI WA JAMII ZABORESHWA NSIMBO DC

Imewekwa: August 26th, 2025

Serikali ya awamu ya sita chini ya Uongozi wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya maboresho makubwa ya huduma za kijamii katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi kwa kuboresha na kujenga miundombinu mingi katika sekta mbalimbali.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bi. Christina Daniel Bunini amesema pamoja na idara zingine, idara ya Afya imeboreshwa katika kipindi cha uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo Halmashauri hiyo imefanikiwa kuongeza vituo vya kutolea huduma za afya hadi kufika 30 ambapo Hospitali ya Wilaya ni moja (1), Vituo vya Afya sita (06) kati ya hivyo, kituo kimoja kinamilikiwa na taasisi binafsi. Pamoja na vituo hivyo vya Afya, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo pia ina Zahanati zipatazo ishirini na tatu (23) zinazohudumia wananchi

Hospitali ya Wilaya ya Nsimbo (Jengo la huduma za dharura)

Kituo cha Afya Itenk ni moja ya Vituo vya kutolea huduma ya Afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo


Kwa upande wa rasilimali watu, Bi Christina Bunini ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ina jumla ya watumishi wa afya 312 sawa na asilimia 42 ya watumishi 742 wanaohitajika kuhudumia wananchi wapatao 201,102 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022. Pamoja na upungufu huo, wataalamu wa afya waliopo wamekuwa wakitekeleza ipasavyo majukumu yao ya kuwahudumia wananchi.

Katika kipindi cha uongozi wa Mheshimwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Idara ya afya imeendelea kuboreshwa kwa kiasi kikubwa kupitia vitengo vyake kama Utawala, Kitengo cha Afya ya Uzazi ya Baba, mama na mtoto, kitengo cha UKIMWI na kifua kikuu, kitengo cha Dawa, vifaa tiba na vitendanishi, kitengo cha huduma za maabara, kitengo cha chanjo na magonjwa yanayotolewa taarifa, kitengo cha Makusanyo ya Fedha na Bima, kitengo cha kudhibiti magonjwa yasiyopewa kipaumbele, kitengo cha kudhibiti Malaria, Magonjwa ya IMCI, kitengo cha afya na mazingira, kitengo cha ustawi wa jamii na kitengo cha huduma ya lishe. Vitengo vyote vimekuwa vikishirikiana katika majukumu mbalimbali jambo linalorahisisha utoaji wa huduma katika jamii kwa urahisi.

Aidha, kwa upande wa Divisheni ya Ustawi wa Jamii, makundi yote maalum ikiwemo wazee, Watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na watu wenye ulemavu yameendelea kuhudumiwa ipasavyo. Pamoja na hayo, Divisheni hii imeendelea pia kushughulikia huduma ya matunzo kwa makundi hayo ikiwemo usuluhishi wa migogoro ya ndoa.

Pamoja na majukumu hayo, idara ya Ustawi wa Jamii pia imeendelea kuratibu shughuli zote zinazofanywa na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayoshughulika na miradi ya UKIMWI, Lishe, Chanjo na Uhifadhi wa mazingira ili miradi yote ilete tija kwa wananchi Wilayani Nsimbo.

Hata hivyo, elimu ya lishe imeendelea kutolewa kwa makundi mbalimbali ya kijamii ikiwemo wajawazito na Watoto wenye umri chini ya miaka mitano, kugawa malighafi za kutengeneza vyakula dawa (F75 na F100) kwenye maeneo ambayo yana idadi kubwa ya watoto walioathirika na utapiamlo.

Hatua ya kujengwa kwa Zahanati na Vituo vya Afya zaidi katika Halmashauri hiyo kumewasaidia wananchi wengi kupata huduma karibu na makazi yao na kupunguza mwendo wa kutembea umbali mrefu wakifuata huduma za afya.

 Katika kupunguza changamoto za usafiri kwa wagonjwa wa dharura katika jamii na kurahisisha huduma kwao, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo imefanikiwa kupata Magari mawili ya kubebea wagonjwa (Ambulance), jambo linalorahisisha usafiri kwa wagonjwa na kuwafikisha katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa haraka

Gari la kubebea wagonjwa (Ambulance)

Matangazo

  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MRADI WA KITUO CHA AFYA IBINDI August 26, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HUDUMA ZA AFYA, LISHE NA USTAWI WA JAMII ZABORESHWA NSIMBO DC

    August 26, 2025
  • BEVAC NSIMBO NA TANGANYIKA YAKABIDHIWA VITUO VYA KUKUSANYIA MAZAO YA NYUKI

    August 19, 2025
  • BEVAC YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA CHAMA CHA USHIRIKA CHA UFUGAJI NYUKI – NSIMBO

    August 13, 2025
  • CRDB BANK YATOA MSAADA WA VITI NA MEZA SITINI KWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa