• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Milioni 122,500,000 zanufaisha Wajasiriamali Nsimbo.

Imewekwa: April 14th, 2021

Pichani:Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh.Jamila Y.Kimaro akikabidhi mfano wa Hundi ya thamani ya Shilingi Mil. 122,500,000.00 kwa Wajasiriamali akina Mama Vijana na Wenye Ulemavu wakati wa Hafla ya kukabidhi mikopo hiyo Aprili 13,2021.katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Nsimbo.


Nsimbo-HQ 

Zaidi ya Wajasiriamali 300 kutoka katika makundi ya kinamama Vijana na wenye ulemavu kutoka kata 12 za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wamenufaika na mkopo  wa Shilingi 122,500,000 (Milioni Mia moja Ishirini na Mbili na Laki tano) ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali la kutenga asilimia 10 za mapato ya ndani kwa ajili ya kuwezesha Wajasiriamali Wanawake Vijana na Wenye Ulemavu kiuchumi  kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

Fedha hizo zimetolewa kwa vikundi 32 ambapo shilingi 57,000,000.00 zimetokana na Asilimia 10 ya mapato ya ndani na kiasi cha Shilingi 65,500,000.00 zimetokana na marejesho ya mikopo kutoka katika vikundi vilivyokopeshwa miaka iliyopita ambapo hadi kufikia Machi 2021 Halmashauri itakuwa imeshatoa jumla ya Tsh. 149,500,000.00 kwa vikundi 39 vya Wajasiriamali  kati ya hivyo vya  Wanawake ni  vikundi 36 na Vijana ni  vikundi 3.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi Hundi kwa Wajasiriamali wanufaika wa mkopo huo Aprili 13, 2021 Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh. Jamila Kimaro amewataka Wajasiriamali wa Nsimbo kutumia fedha hizo kwa malengo mahsusi ili kufikia azma ya Serikali kuwakwamua Wananchi waweze kuondokana na Umasikini.

Mh.Kimaro amebainisha kuwa sababu kubwa inayopelekea baadhi ya vikundi vya wajasiriamali Nchini kushindwa ni pamoja na kushindwa kutumia fedha kwa ajili ya malengo mahsusi jambo linalopelekea changamoto ya kutorejesha mikopo kwa Wakati.

Ameeleza kuwa ni muhimu kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii Nsimbo kushirikiana kwa karibu na Viongozi wa Kisiasa kusudi Elimu iweze kuwafikia  watu wa makundi mbalimbali ikiwemo makundi maalumu ya Walemavu ambao kwa Nsimbo  wameonyesha muitikio mdogo kushiriki katika fursa hii muhimu iliyotolewa na Serikali.

Aidha Mh.Kimaro ameupongeza Uongozi wa Halmashauri kwa usimamizi makini wa kuhakikisha kuwa fedha za Mikopo zinarejeshwa kwa wakati na  hivyo kuwezesha makundi mengine  kukopa hatua ambayo inatoa fursa kwa engine kunufaika na fursa hiyo.

Awali akimkaribisha mgeni rasmi katika Hafla hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya  Nsimbo Bw.Mohamed Ramadhani  amewataka Wajasiriamali kuwekeza zaidi katika elimu na ujuzi wa biashara kabla ya kuchukua Mikopo.

Ameeleza kuwa fedha pekee haiwezi kuleta matunda yaliyokusudiwa ikiwa Elimu ya biashara kwa Wajasiriamali,haitotolewa na hivyo kuwataka Wajasiriamali hao kuwekeza zaidi katika kutafuta maarifa na Elimu ya Biashara ili waweze kupata faida

Amesema ni muhimu kwa Wajasiriamali kutanua wigo wa biashara kwa kuondokana na biashara za muda mfupi na badala yake walenge kuanzisha biashara za Uwekezaji ili waweze kujikwamua na umasikini.

Amesisitiza Wajasiriamali kuhakikisha kuwa mitaji inakua, kuzingatia muda wa marejesho sambamba na kutoa hamasa na elimu kwa wengine ili waweze  kukopa kwa wingi ili kutoa fursa kwa wengi waweze kunufaika.


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa