• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

MKURUGENZI MTENDAJI NSIMBO AKABIDHI MIZINGA KWA WANACHAMA WA CHAMA CHA USHIRIKA WA MAZAO YA NYUKI

Imewekwa: July 10th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Bi. Christina Bunini, amekabidhi mizinga kwa wanachama wa Chama cha Ushirika wa Mazao ya Nyuki kama sehemu ya juhudi za kuongeza uzalishaji na kuinua sekta ya ufugaji nyuki katika wilaya hiyo. Tukio hilo limefanyika wakati wa ziara ya kikazi ya Mradi wa BEVAC, unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya kupitia shirika la Enabel, kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Bi. Bunini amesema hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Serikali na wadau wa maendeleo ya kuimarisha miundombinu ya sekta ya nyuki, sambamba na kuwawezesha wanavikundi kwa vitendea kazi muhimu ili kuongeza tija na kipato.

Ziara hiyo iliyoongozwa na Mratibu wa Mradi wa BEVAC, Bi. Flosia Vugo, imelenga kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha usindikaji wa mazao ya nyuki pamoja na kujionea namna wanachama wanavyoongeza thamani ya mazao yao kwa kutumia mbinu bora na zenye tija.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama, Bw. Peter Kalula, alisema chama hicho kilianza mwaka 2022 kikiwa na wanachama 80 na hadi Julai 2025 wamefikia wanachama 170, ikiwa ni pamoja na wanawake 30. Alisema ongezeko hilo linaonesha hamasa kubwa kutoka kwa jamii na uwezo wa sekta ya nyuki kubadilisha maisha ya wananchi.

Hata hivyo, alitaja changamoto kama vile umbali wa ofisi za utoaji vibali, gharama kubwa za vibali, na ukosefu wa masoko ya uhakika kwa bidhaa zao. Alitoa wito kwa Serikali na Mradi wa BEVAC kusaidia upatikanaji wa mikopo na kufungua masoko ya kudumu.

Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji, Bw. Kayumba Torokoko, aliwapongeza wanachama kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa kituo na akawahimiza kuanzisha vyanzo mbadala vya mapato ili kujiimarisha kiuchumi.


Mradi wa BEVAC umeendelea kuonyesha dhamira ya kuinua sekta ya ufugaji nyuki kwa kusaidia uboreshaji wa miundombinu, kutoa mafunzo ya kitaalamu, na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali, wadau wa maendeleo, na jamii. Kwa msaada huu endelevu, ndoto za wananchi wa Nsimbo kushiriki kikamilifu katika mnyororo wa thamani wa mazao ya nyuki zinaendelea kutimia.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • NSIMBO YATOA MAFUNZO KWA WATENDAJI KUHUSU ANWANI ZA MAKAZI NA POSTKODI

    July 10, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI NSIMBO AKABIDHI MIZINGA KWA WANACHAMA WA CHAMA CHA USHIRIKA WA MAZAO YA NYUKI

    July 10, 2025
  • SAMIA DAY: KATAVI YAANDAA TAMASHA KUBWA KUADHIMISHA MIAKA MITANO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    July 02, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE (LAAC)

    June 19, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa