• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

NSIMBO YAENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Imewekwa: November 28th, 2025

Timu ya Tathmini na ufuatiliaji wa miradi ya Maendeleo (M&E) katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi imeendelea kufanya ziara ya ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Miradi iliyotembelewa leo na kukagauliwa ni pamoja na Ukarabati wa Soko la Sonambele iliyopo katika Kata ya Kapalala, ambapo kiasi cha shilingi milioni 20 zilipelekwa kwaajili ya ukarabati na ujenzi wa vizimba katika soko hilo, ambapo hadi sasa ujenzi uko katika hatua ya umaliziaji.

Mradi mwingine ni mradi wa Ukarabati wa Zahanati ya Kajeje, ambapo kiasi cha shilingi milioni 20 zilipelekwa huko kukamilisha mradi huo, Ambapo hadi sasa mradi huo uko katika hatua ya umaliziaji. Aidha, mkandarasi anayetekeleza mradi huo amepewa muda wa wiki moja kuhakikisha kazi zilizobaki, ikiwa ni pamoja na kupiga msasa na kupaka rangi zimekamilika ndani ya wiki moja.

Aidha, Katika mradi wa Ukarabati wa vyoo katika Soko la Kanoge, timu hiyo imefanya ukaguzi wa matundu 12 ya vyoo katika soko la Kanoge ambapo ukarabati wa vyoo hivyo unatarajia kufanyika kwa haraka na mradi huo unatarajia kukamilika kabla ya tarehe 31 desemba 2025. Kiasi cha shilingi milioni 10 zimetengwa kwaajili ya mradi huo.

Timu hiyo imeendelea na ukaguzi katika mradi mwingine ambao ni mradi wa Ujenzi wa Shule mpya ya Awali na Msingi, unaotekelezwa katika Kijiji cha Katambike Kata ya Ugalla. Katika mradi huu, kiasi cha shilingi milioni 342.9 zimepelekwa kwaajili ya mradi huu, ambapo hadi sasa ujenzi wa Jengo la Utawala na majengo yenye jumla ya Madarasa 6 ya elimu msingi unaendelea na upo katika hatua ya jamvi.

Mradi mwingine ni mradi wa umaliziaji wa nyumba ya watumishi yenye uwezo wa kutumiwa na familia mbili za watumishi yaani (2 in 1) katika Shule ya Sekondari Ugalla River. Katika Mradi huu, kiasi cha shilingi milioni 40 zilipelekwa katika mradi huo ambapo hadi sasa mradi huo uko katika hatua za mwisho kukamilika ambapo mkandarasi amepewa wiki moja kukamilisha kazi ya upigaji rangi na kuweka marumaru ili mradi huu uanze kutumika.

Aidha, timu hiyo ilifika katika mradi mwingine wa Stendi ya Mabasi katika kata ya Ugalla, Timu imetembelea na kukagua eneo la mradi wa ujenzi wa stendi ya mabasi katika kata ya Ugalla ambapo ukaguzi umefanyika katika hatua ya awali hasa mipaka ya eneo lililotengwa kwaajili ya mradi huo.

Aidha, mradi mwingine ni mradi wa Umaliziaji wa Majengo katika Kituo cha Afya Ugalla. Ambapo katika mradi huu, Kiasi cha sh. milioni 40 zilipelekwa kwajili ya umaliziaji wa miundombinu katika jengo la Mama na Mtoto, Maabara na Jengo la wagonjwa wa nje. Hadi sasa jengo la mama na mtoto pamoja na jengo la upasuaji na wodi ya wanawake limekamilika.

Katika miradi yote iliyotembelewa na timu hiyo, wajumbe waliongonzwa na Bwana Julius Moshi aliyemwakilisha Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bi. Christina Bunini waliwasihi wakandarasi kuongeza kasi ili kukamilisha miradi hiyo kwa haraka na kwa viwango vinavyotakiwa na hatimaye miradi hiyo ianze kutumika na kuwasaidia wananchi.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA KIDATO CHA KWANZA 2026 December 04, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MRADI WA KITUO CHA AFYA IBINDI August 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA November 13, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA NSIMBO YAPELEKA NEEMA KWA WAFANYABIASHARA, WANANCHI KIJIJI CHA MAGULA

    January 22, 2026
  • RC MRINDOKO AHIMIZA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO – NSIMBO DC

    December 17, 2025
  • KAMATI YA SIASA MPANDA YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO H/W NSIMBO

    December 19, 2025
  • DC MPANDA AHIMIZA UANDIKISHAJI WA WANAFUNZI WA AWALI NA MSINGI

    December 10, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa