Katika jitihada za kukabiliana na tishio la wimbi la tatu la Ugonjwa Korona Nchini, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kupitia Ofisi ya Mganga mkuu wa Wilaya Nsimbo imeendelea kuratibu na kuandaa mikakati mbalimbali ya kukabiliana na Ugonjwa huo lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa Wananchi wanakuwa salama na tahadhari zinaendelea kuchukuliwa.
Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauriya Wilaya ya Nsimbo Bw.Wambura Warioba amesema katika jitihada za kukabiliana na tishio la Wimbi la Tatu la Ugonjwa wa Korona Halmashauri imejipanga kutoa elimu na hamasa kwa Wananchi lengo likiwa ni kujenga uelewa juu ya namna ya kujikinga na Ugonjwa huo
Dkt.Warioba amesema tayari Halmashauri imeanza kutoa Elimu kwa Watumishi wa kada mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ambapo Watumishi wa Makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wamejengewa uwezo wa namna ya kujikinga na Ugonjwa huo wa Korona
Aidha Dkt.Warioba amesema Elimu na Hamasa itaendelea kutolewa kwa Wananchi juu ya mbinu na njia mbalimbali za Kisayansi zinazopaswa kutumika kujikinga ana Ugonjwa wa Korona ambapo timu ya Elimu na Hamasa itazunguka katika maeneo yote ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo
Amesema ni muhimu kwa Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Ugonjwa wa Korona kwa kuhakikisha kuwa Wanavaa Barakoa kwa usahihi katika maeneo yote ya mikusanyiko hususani masoko,zahanati,Shuleni na katika nyumba za Ibada ili kudhibiti kuenea kwa Ugonjwa huo.
Ameeleza kuwa endapo Wananchi watazingatia njia zote za Kitaalam za kukabiliana na Ugonjwa wa Korona Mkoa wa Katavi na Nsimbo kwa Ujumla utabaki salama.
Mpanda to Tabora road
Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda
Simu : 025 295 5164
Simu: 025 295 5164
Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz
Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa