• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

PREMIUM ACTIVE YAUNGA MKONO ELIMU, YATOA MADAWATI 201 NSIMBO

Imewekwa: February 25th, 2025

Kampuni ya Premium Active (T) Limited, inayojihusisha na ununuzi wa tumbaku, imekabidhi madawati 201 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kama sehemu ya mchango wake kwa jamii, hatua inayolenga kupunguza uhaba wa madawati mashuleni.

Makabidhiano hayo yamefanyika katika hafla iliyofanyika katika kijiji cha mwenge kilichopo katika kata ya Nsimbo, ikihudhuriwa na viongozi wa serikali na sekta binafsi. Mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Mhe. Jamila Yusuph Kimaro, ameipongeza kampuni hiyo kwa kuunga mkono juhudi za serikali za kuboresha elimu na kusaidia wanafunzi kupata mazingira bora ya kujifunzia.

Baada ya kupokea madawati hayo, Mhe. Kimaro alimkabidhi rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nsimbo, Bi. Christina Daniel Bunini, ambaye ameahidi kuyasambaza kwa shule  zilizopo katika kata zenye uzalishaji wa zao la  tumbaku ambazo alizitaja kuwa ni kata ya Katumba, Kanoge, na Ugalla. Miongoni mwa shule zitakazonufaika ni Bulembo, Kabuga, Kalungu, Kanoge, Kasisi, Lukama, Mtambo ambazo zitapewa  idadi sawa ya madawati 25 huku  Ivungwe ikipatiwa madawati 26.

Aidha  ameagiza waalimu katika shule hizo kuyatunza madawati ikiwa ni pamoja na kuyafanyia  ukarabati pale inapotakiwa.

Kwa mujibu wa Afisa Uzalishaji wa Premium Active Tanzania, Bw. Frank Ayoh, msaada huo ni sehemu ya utaratibu wa kampuni wa kurejesha asilimia 6 kwa kila kilo ya tumbaku inayouzwa. “Tuliwasiliana na idara ya elimu na kubaini kuwa mahitaji makubwa ni madawati, hivyo tumechangia shilingi milioni 14.7 kusaidia wanafunzi wa Nsimbo,” alisema.

Mkuu wa Kitengo cha Elimu Msingi, Bw. Frank Sichalwe, amesema madawati hayo yamechangia kupunguza uhaba uliokuwepo wa madawati 5,312. “Tunatoa wito kwa makampuni mengine kuiga mfano huu kwa kusaidia sekta ya elimu,” aliongeza.

Wanafunzi walionufaika na msaada huo wameeleza furaha yao, wakiahidi kuyatunza madawati kwa ajili ya vizazi vijavyo.  Kasanga Ramadhani, aliyewakilisha wanafunzi, alisema: “Tutahakikisha tunawahamasisha wenzetu kuyatunza madawati haya kwa ustawi wa baadaye.”


Serikali imeendelea kusisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya sekta binafsi na umma ili kuboresha mazingira ya elimu na kuhakikisha kila mwanafunzi anapata nafasi ya kusoma katika mazingira rafiki.


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa