• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Ujenzi Sekondari ya Wasichana Kapalala katika hatua nzuri,CMT Nsimbo wafuatilia kwa karibu Ujenzi.

Imewekwa: February 12th, 2022

Pichani:Hali ya Ujenzi wa Jengo la Utawala,ikiwa ni  moja kati ya Majengo katika Mradi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Kapalala Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo hadi kufikia 11 Februari 2022.

Na: John Mganga DIO 

Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana unaoendelea katika Kata ya Kapalala Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo umeendelea kwa kasi ya kuridhisha huku Menejimenti ya Halmashauri ikifuatilia kwa karibu Maendeleo ya Ujenzi huo.

Hadi kufikia Tarehe 12, Februari 2022, Majengo yote katika mradi huo yameanza kupandishwa pasi kuwepo na changamoto yeyote inayoathiri Ujenzi huo ambapo shughuli za Ujenzi zimekua zikisimamiwa kwa karibu na Kamati ya Ujenzi ya Kata ya Kapalala ambayo wajumbe wake muda wote wameonekana wakiwa katika eneo la Ujenzi.

Tangu kuanza utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo Tarehe 5 Februari 2022 Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ikiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji kwa sasa Bi. Tabia Nzowa kwa siku zote za wiki wametembelea eneo hilo kwa lengo la kujiridhisha na maendeleo ya Ujenzi wa mradi huo.

Pamoja na Wataalamu wengine,Februari 11, 2022 Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya  Nsimbo Bw.Elisonguo Mshiu alifika eneo la mradi kwa lengo la kukagua maendeleo ya Ujenzi na kuzungumza na Kamati ya Ujezi pamoja na  Mafundi wazawa wanaotekeleza mradi huo kwa lengo la kubaini iwapo kuna changamoto yeyote katika eneo la Ujenzi kusudi  ipatiwe ufumbuzi mara moja.

Bw.Mshiu amewahakikishia mafundi wanaotekeleza Ujenzi wa Mradi huo kuwa Halmashauri inafuatilia kwa karibu Ujenzi huo  na kwamba Menejimenti  inafanya ufuatiliaji kwa karibu zaidi ili endapo kutatokea changamoto yoyote basi ipatiwe ufumbuzi kwa wakati ili kutoathiri kasi ya Ujenzi huo.

Amewataka wajumbe wa Kamati ya Ujenzi ya Mradi huo kusimamia kwa karibu na kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mafundi ili kuhakikisha kuwa Mradi huo unakamilika kwa ubora ,viwango vinavyotakiwa na  kwa wakati uliopangwa huku akiwataka kuelekeza nguvu kubwa zaidi katika kulinda vifaa vya Ujenzi vilivyopo katika eneo hilo la Ujenzi.

Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kapalala katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo unaotekelezwa kwa fedha za Mpango wa Kuinua ubora wa Elimu ya Sekondari Nchini SEQUIP T unahusisha Vyumba Nane vya Madarasa,Maabara tatu,Jengo la Utawala,Maktaba moja,Chumba cha TEHAMA pamoja na matundu Ishirini ya Vyoo.

Serikali kupitia mpango wa kuinua Ubora wa Elimu ya Sekondari SEQUIP T ilitenga Kiasi cha Shilingi Milioni 600 kwa ajili ya Ujenzi wa Sekondari hiyo ya Wasichana ambapo hadi sasa Shilingi Milioni 470 zimekwisha tolewa kwa ajili ya kutekeleza Mradi huo unaotarajiwa kukamilika ifikapo Tarehe 08, Agosti 2022.

Picha 1:Hali ya Ujenzi wa Jengo la Utawala katika Mradi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Kapalala hadi kufikia 11 Februari 2022.


Picha 2:Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Bw.Elisonguo Mshiu akitoa maelekezo kwa viongozi wa Kamati ya Ujenzi ya Kata ya Kapalala alipofanya ukaguzi katika eneo la Mradi 11 Februari 2022


Picha 3;Hali ya Ujenzi katika moja kati ya Vyumba 8 vya Madarasa katika Mradi wa Ujenzi wa  Shule ya Sekondari ya Wasichana Kapalala hadi kufikia 11 Februari 2022


Picha4;Hali ya Ujenzi wa moja kati ya Vyumba 3 vya Maabara katika Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana  Kapalala hadi kufikia 11 Februari 2022

Picha 5;Stoo ya kuhifadhia Vifaa vya Ujenzi katika Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kapalala



Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa