Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh.Onesmo Buswelu akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Mafunzo ya Anuani za Makazi katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Nsimbo Februari 15,2022
Nsimbo-Mtapenda
Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wakiwemo Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya,Wakuu wa Idara na Vitengo,Madiwani , Watendaji wa Vijijiji na Kata pamoja na Wenyeviti wa Vijiji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo,wametakiwa kuwa wazalendo na kutanguliza maslahi ya Taifa mbele wakati wa utekelezaji wa zoezi la uwekaji mfumo wa anuani za makazi.
Rai hiyo imetolewa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Onesmo Buswelu alipofungua Mafunzo ya kuwajengea uwezo Viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo juu ya namna ya kutekeleza zoezi la uwekaji mfumo wa anuani za makazi.
DC Buswelu amesema ili zoezi hilo liweze kutekelezwa kwa ufanisi ni vema Viongozi wakatimiza wajibu wao kwa kutoa ushirikiano wa kutosha ili kukamilisha zoezi hilo ambalo linafanyika Nchi Nzima.
Awali akitoa maelezo kuhusu Mfumo wa anuani za Makazi unavyofanya kazi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bi Tabia Nzowa ameeleza kuwa Serikali imedhamiria kuweka Anwani za Makazi kwa nchi Nzima; ili kurahisisha upatikanaji, utoaji na ufikishaji wa huduma katika maeneo mbalimbali.
Bi Tabia ameeleza kuwa Mfumo wa anuani za makazi utatoa utambulisho wa mahali, mtu au kitu kilipo juu ya uso wa Nchi ambapo ametaja manufaa ya Mfumo huo kuwa ni pamoja na kuwezesha ufanyikaji wa baishara mtandao,kuboresha upataji,utoaji na upelekaji wa huduma na bidhaa mahala stahiki,kuimarisha ulinzi na Usalama,Uborshaji wa ukusanyaji wa mapato,kurahisisha shughuli za utafiti na upatikanaji wa Taarifa.
Aidha Bi Tabia ameeleza kuwa Halmashauri inabeba jukumu la kupanga, kupima, kugawa, kumilikisha na kusimamia uendelezaji wa makazi na uundaji wa anwani utakaorahisha utambuzi wa maeneo ya Makazi, barabara na njia zinazowezesha kufika maeneo yote na hivyo kuwataka Viogozi na Wataalamu kushirikiana vema ili kufanikisha zoezi hilo.
Mada zilizowasilishwa katika mafunzo hayo ni pamoja na Maana ya Mfumo wa anuani za Makazi na Postikodi,Utambuzi wa Barabara na Ugawaji wa Namba,Uwekaji namba kwenye makazi,Aina za Vibao kwenye nyumba na barabara,namna ya kutumia na kuingiza Taarifa kwenye Mfumo,pamoja na Mafunzo kwa Vitendo ambapo Washiriki walitembelea maeneo mbalimbali ya Mitaa kwa lengo la kujifunza kwa vitendo namna ambavyo vibao vya barabara na mwenye nyumba vitawekwa.
Mpanda to Tabora road
Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda
Simu : 025 295 5164
Simu: 025 295 5164
Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz
Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa