• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

WAJASIRIAMALI KUNUFAIKA NA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO

Imewekwa: July 23rd, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mheshimiwa  Jamila Yusuph amekabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi Milioni mia nne na ishirini (M420) pamoja na pikipiki kumi na moja (11) kwa wajasiriamali wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi katika hafla ya utoaji wa mikopo ya asilimia kumi kutoka mapato ya ndani inayotolewa na halmashauri. Hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa shule ya sekondari Nsimbo Mkoani Katavi imehudhuriwa na vikundi hamsini na sita vya wajasiriamali walionufaika na mkopo huo.

Mheshimiwa Jamila Yusuph amewasihi wajasiriamali hao walionufaika na mikopo hiyo kutumia fedha hizo kwa miradi na malengo yaliyokusudiwa ili kuepuka changamoto wakati wa urejeshwaji. Katika hafla hiyo, takribani vikundi hamsini na sita vilivyosajiliwa ikijumuisha makundi ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu wamepokea kwa furaha mikopo hiyo inayolenga kuwainua kiuchumi.

Katika kuimarisha usimamizi na uendeshwaji wa miradi iliyokusudiwa na wajasiriamali hao, Mheshimiwa Jamila Yusuph amewakumbusha maafisa maendeleo ya jamii katika ngazi zote halmashauri ya wilaya ya Nsimbo kuendelea kuwatembelea wanufaika hao na kutoa elimu ili wayafikie matarajio yaliyopangwa wakati wa uombaji wa mikopo hiyo ili kusudi iwe na tija kiuchumi.

Mheshimiwa Jamila amewatia moyo waombaji waliokosa fursa ya mikopo hiyo kutokata tamaa kwani serikali bado inaendelea kutenga fedha kwaajili ya makundi lengwa kila mwaka, hivyo waendelee kujishughulisha wakati wakisubiri fursa hiyo wakati mwingine kwakuwa wombaji ni wengi na bajeti ni ndogo, jambo lililosababisha baadhi ya waombaji kukosa mikopo hiyo.

Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Wilaya ya Mapanda mheshimiwa Jamila Yusuph ametumia fursa hiyo kukemea vitendo vya ukatili vinavyotokea katika jamii hasa vikihusisha makundi ya watoto na wanawake. Amewakumbusha wazazi kuendelea kuwalinda watoto hasa kwa kukaa na kuwa karibu na watoto wao ili iwe rahisi kufahamu viashiria vya ukatili na changamoto zingine wanazopitia katika familia, jamii na hata mashuleni ili kuwasaidia mapema kabla hayajawathiri.

Aidha, Mheshimiwa Jamila amewakumbusha wananchi Wilayani Nsimbo kuzingatia lishe bora ili wawe na afya njema na imara na hivyo kutekeleza majukumu yao kwa wakati na kwa weledi mkubwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bi. Christina Bunini amewasihi wanufaika wa mikopo hiyo kufanya marejesho bila kufuatiliwa wala kusuasua ili iweze kuwanufaisha waombaji wengine kwa wakati kama ambavyo wao wamepata fursa hiyo.

Wakati huohuo Bi. Christina Bunini amewaasa wanufaika wa mikopo hiyo hasa kundi la maafisa usafirishaji (bodaboda) kuendesha pikpiki kwa tahadhari muda wote wakiwa katika hali ya utimamu wa mwili na akili ili kuepusha ajali zinazoepukika.

Kabla ya makabidhiano ya mfano wa hundi, akitoa taarifa ya mwenendo mzima wa mikopo hiyo, Mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bwana Rodrick Kidenya amesema jumla ya vikundi mia moja na nne (104) vilijitokeza kuomba mikopo hiyo ambapo viliomba jumla ya shilingi bilioni moja na milioni mia saba (Bilioni 1.7).

Bwana Kidenya amesema kulingana na ufinyu wa bajeti, ni vikundi hamsini na sita tu ndivyo vilivyopewa kipaumbele na kukabidhiwa mikopo hiyo ambapo wanapaswa kurejesha ndani ya mwaka mmoja.

Awali akitoa elimu kwa vikundi hivyo, Afisa Maendeleo ya Jamii Kata ya Kanoge Wilayani Nsimbo Bi. Hollo Mbagga amekumbusha wajasiriamali hao namna bora ya kusimamia rasilimali, ikiwa ni pamoja na ushirikiano ulio bora, mawasiliano kwa wakati, ufuatiliaji na tathmini pamoja na kutochoka kujifunza ili kuboresha miradi yao waliyokusudia kuianzisha.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na Katibu tawala wa Wilaya ya Mpanda  Bwana Juma Abdalla, wanufaika kutoka jumla ya vikundi hamsini na sita wamekabidhiwa mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni mia nne na ishirini pamoja pikipiki kumi na moja kwaajili ya kundi la maafisa usafirishaji.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kutokomeza udumavu

    July 29, 2025
  • WAJASIRIAMALI KUNUFAIKA NA MIKOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO

    July 23, 2025
  • MKURUGENZI MTENDAJI NSIMBO AONGOZA MAZOEZI YA JOGGING KWA WATUMISHI NA WANANCHI

    July 12, 2025
  • NSIMBO YATOA MAFUNZO KWA WATENDAJI KUHUSU ANWANI ZA MAKAZI NA POSTKODI

    July 10, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa