• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPEWA MAFUNZO - JIMBO LA NSIMB0

Imewekwa: August 4th, 2025

Kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba 2025, Wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata katika Jimbo la Nsimbo Mkoani Katavi wamepewa mafunzo elekezi yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani humo. Akifungua mafunzo hayo, msimamizi wa uchaguzi katika Jimbo la Nsimbo Bwana Julias Zakaria Moshi amewataka wasimamizi wasaidizi hao kufuata Sheria, kanuni, taratibu na miongozo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Bwana Moshi amewakumbusha wasimamizi hao wasaidizi ngazi ya Kata kufuatilia kwa umakini mafunzo yanayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili wawe watendaji wazuri na waendelee kuwa wazalendo, waaminifu na kufanya kazi kwa uadilifu kwa kufuata viapo vyao kwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Aidha, amewataka wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Kata kuvishirikisha vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote kwa kuzingatia matakwa, sheria, kanuni na maelekezo mbalimbali ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Sambamba na hayo, Bwana Moshi amewataka wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata kusoma kwa makini Katiba, sheria, kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yatakayotolewa na Tume na kuuliza ili kupata ufafanuzi wa jambo lolote litakaloonekana kuwa na changamoto katika utekelezaji wa majukumu waliyopewa.

Kabla ya kufunguliwa kwa mafunzo hayo, Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Kata wamekula kiapo cha kutunza siri na kujivua uanachama kwa waliokuwa wanachama wa vyama vya siasa kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu 2025

Itakumbukwa kwamba, Tuma Huru ya Tiafa ya Uchaguzi imetangaza Siku ya Jumatano ya taerehe 29/10/2025 kuwa siku ya Uchaguzi mkuu, ambapo watanzania wenye sifa watatumia haki yao ya kikatiba ya kuchagua Rais, wabunge na madiwani.


KURA YAKO HAKI YAKO, JITOKEZE KUPIGA KURA



Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • BEVAC YAKABIDHI VIFAA VYA TEHAMA KWA CHAMA CHA USHIRIKA CHA UFUGAJI NYUKI – NSIMBO

    August 13, 2025
  • CRDB BANK YATOA MSAADA WA VITI NA MEZA SITINI KWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KATAVI

    August 12, 2025
  • NSIMBO YAPOKEA SHILINGI BILIONI 1.01 KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO KATIKA BAJETI YA 2025/2026 KUTOKA SERIKALI KUU

    August 05, 2025
  • WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA WAPEWA MAFUNZO - JIMBO LA NSIMB0

    August 04, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa