• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA WAZINDULIWA RASMI NSIMBO, MKOANI KATAVI

Imewekwa: June 9th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko, ameongoza sherehe ya uzinduzi wa msimu wa ununuzi wa pamba na mazao mengine kwa mwaka 2025/2026, hafla iliyofanyika katika Kijiji cha Kapalala, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo. Tukio hilo limehudhuriwa na viongozi wa serikali, vyama vya ushirika (AMCOS), wakulima, na wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo.

Katika hotuba yake, Mhe. Mrindoko amewataka wakuu wa wilaya kusimamia kwa karibu uuzaji wa mazao kupitia vituo na mifumo rasmi ya serikali ili kudhibiti uuzaji holela unaosababisha hasara kwa wakulima pamoja na uhaba wa chakula majumbani.

Amesisitiza kuwa mazao ya pamba na tumbaku—yanayohusisha wakulima wengi mkoani humo—yanapaswa kuendeshwa chini ya usimamizi makini wa vyama vya msingi vya ushirika. Ameeleza kuwa baadhi ya viongozi wa vyama wamekuwa wakikiuka taratibu kwa kuingia mikataba isiyo rasmi na wakulima, jambo linalowaumiza wakulima kibiashara. Hivyo, amewaagiza wakuu wa wilaya kuhakikisha kilimo cha mkataba kinasimamiwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na miongozo ya serikali.

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa ametangaza kuwa Katavi itaanza kutumia mfumo wa stakabadhi ghalani, kuanzia na zao la ufuta katika msimu huu wa 2025/2026. Amehimiza wakulima kuunga mkono mfumo huo kwa kuwa unalenga kutoa bei nzuri, usalama wa soko, na kupunguza unyonyaji kutoka kwa walanguzi.

Aidha, ameipongeza kampuni ya NGS Investment Company Ltd kwa kuendelea kuwa soko la uhakika la zao la pamba mkoani humo. Amewataka wakulima kuhakikisha wanachuma pamba kwa usafi, kuipepeta vizuri na kuifikisha sokoni ikiwa katika ubora unaokubalika ili kukidhi mahitaji ya soko.

Akizungumza kwa niaba ya Bodi ya Pamba, Bw. Bugelaha Filbert amesema kuwa ili mkulima anufaike na kilimo cha pamba, ni lazima azalishe kwa tija—kwa kutumia mbegu bora, mbolea, na matunzo sahihi. Amesema kuwa mkulima anaweza kuvuna hadi kilo 1,000 kwa hekari moja ikiwa atazingatia kanuni hizo.

Kwa upande wao, wananchi waliohudhuria hafla hiyo wameeleza kufurahishwa na kuanza kwa msimu mpya wa ununuzi wa pamba, wakisema kuwa matumizi ya mizani bora na ya kisasa yameongeza matumaini ya kupata haki katika vipimo. Wameiomba serikali kuhakikisha kuwa malipo ya pamba yanafanyika kwa wakati ili kuwawezesha kujipanga kwa msimu mwingine wa kilimo na shughuli za kijamii.

Katika kauli yake ya mwisho, Mkuu wa Mkoa Mhe. Mrindoko amewahimiza vijana wa Katavi kutumia msimu huu kama fursa ya kuwekeza kwenye kilimo, akisisitiza kuwa ni sekta inayotoa ajira, kipato, na mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa.

Kapalala, Nsimbo – Juni 9, 2025

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SAMIA DAY: KATAVI YAANDAA TAMASHA KUBWA KUADHIMISHA MIAKA MITANO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    July 02, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE (LAAC)

    June 19, 2025
  • MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA WAZINDULIWA RASMI NSIMBO, MKOANI KATAVI

    June 09, 2025
  • KAMPENI YA MWEZI WA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    June 01, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa