• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

SAMIA DAY: KATAVI YAANDAA TAMASHA KUBWA KUADHIMISHA MIAKA MITANO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

Imewekwa: July 2nd, 2025

Mkoa wa Katavi umeandaa tamasha kubwa la Samia Day kwa lengo la kuadhimisha na kutangaza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano ya Serikali ya Awamu ya Sita, chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 4 hadi 5 Julai, 2025, katika Viwanja vya Shule ya Msingi Inyonga, Halmashauri ya Wilaya ya Mlele. Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mheshimiwa Mwanamvua Hoza Mrindoko.

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 2, 2025, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela, alisema kuwa lengo kuu la tamasha hilo ni kumpongeza na kumshukuru Rais Samia kwa mchango wake mkubwa wa kuleta maendeleo mkoani humo, ambapo zaidi ya shilingi trilioni 1.3 zimetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Kaulimbiu ya tamasha hili ni: ‘Asante Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Fedha za Maendeleo; Katavi Imara, Maendeleo Imara’. Tukio hili linahusisha Serikali ya Mkoa wa Katavi, taasisi mbalimbali na kundi maalum la burudani linalojulikana kama Mkasi Utaongea,” alisema Msovela.

Tarehe 4 Julai, 2025, timu ya Mkasi Utaongea, viongozi wa Serikali na wataalam mbalimbali watatembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi kujionea vivutio vya utalii na kufanya ziara kwenye miradi ya kimkakati ikiwemo Mradi wa Maji wa Miji 28 – Shanwe, vihenge vya kisasa vya kuhifadhia mazao, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa na kituo cha kupozea umeme kutoka Grid ya Taifa.

Katika siku hiyo pia kutafanyika ‘Usiku wa Mama Samia’ katika Ukumbi wa Mpanda Social Hall, ambapo viongozi na wadau mbalimbali watapata fursa ya kujadili maendeleo ya Mkoa – tulikotoka, tulipo, na tunakoelekea.

Kilele cha Samia Day kitafanyika Julai 5, 2025, ambapo shughuli zitaanza na matembezi ya hiari kuanzia saa 1:30 asubuhi katika Mji wa Inyonga, yakiongozwa na Mkuu wa Mkoa, Mheshimiwa Mrindoko.

Michezo na burudani zitakazofanyika ni pamoja na mpira wa miguu, kuvuta kamba, kukimbia kwa magunia, kufukuza kuku na mbio za mita 100.

Msovela alitoa wito kwa wananchi wote wa Mkoa wa Katavi kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye tamasha hili la kihistoria, huku akihimiza ushiriki wa makundi yote ya jamii ikiwemo bodaboda, bajaji, mama lishe, machinga, wasanii na wananchi wote kwa ujumla.

Alizitaka pia taasisi za Serikali na zisizo za Serikali, mashirika ya kiraia, sekta binafsi na wadau wa maendeleo kushiriki kwa pamoja katika maadhimisho haya, kama ishara ya mshikamano na shukrani kwa mafanikio yaliyopatikana

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SAMIA DAY: KATAVI YAANDAA TAMASHA KUBWA KUADHIMISHA MIAKA MITANO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    July 02, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE (LAAC)

    June 19, 2025
  • MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA WAZINDULIWA RASMI NSIMBO, MKOANI KATAVI

    June 09, 2025
  • KAMPENI YA MWEZI WA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    June 01, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa