• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

USHIRIKIANO WA JAMII NA VIONGOZI WA SERIKALI KUONDOA UDUMAVU NSIMBO

Imewekwa: May 30th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Bi. Christina Daniel Bunini,  ametoa wito kwa ushirikiano wa dhati kutoka kwa viongozi wa kata, vijiji, idara mbalimbali pamoja na jamii kwa ujumla ili kufanikisha mapambano dhidi ya tatizo la udumavu.

Akizungumza wakati wa kufunga kikao cha Kamati ya Lishe kwa robo ya tatu ya mwaka kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa Halmashauri, Bi. Christina Bunini amesema kuwa mafanikio katika vita dhidi ya udumavu yanahitaji juhudi za pamoja na mshikamano wa kijamii, hasa katika ngazi ya familia.

“Vita dhidi ya udumavu inahitaji kila mmoja wetu kushika ‘bunduki’ yake – iwe ni elimu, usimamizi, ushirikishwaji wa jamii au rasilimali – ili tufanikishe mapinduzi ya lishe,” alisisitiza Bi. Bunini mbele ya wajumbe wa kamati hiyo na wadau mbalimbali wa sekta ya lishe na afya.

Katika kikao hicho, wajumbe wamejadili kwa kina changamoto zinazosababisha udumavu pamoja na kutoa mapendekezo mahsusi ya kuboresha utekelezaji wa afua za lishe katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri.

Bunini pia ameagiza kuanzishwa kwa kampeni maalum ya kuwahamasisha wazazi kushiriki katika utoaji wa chakula shuleni, kufuatia taarifa kuwa ni asilimia 53 tu ya shule zinazotoa chakula kwa wanafunzi – hali inayochangiwa na mwitikio mdogo wa baadhi ya wazazi.

Kwa upande wake, Afisa Lishe wa Wilaya, Bw. Nikson Johanes, amesema kuwa mafanikio ya mkakati wa lishe hayawezi kufikiwa bila ushiriki wa jamii, akibainisha kuwa uelewa na ushirikiano wa karibu na wananchi ni nyenzo muhimu ya kuinua afya ya watoto.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji amemwagiza Mganga Mkuu wa Halmashauri, Dkt. Bonifasi Masaga (aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo), kuhakikisha kuwa bajeti inatengwa mahsusi kwa ajili ya kuwawezesha watoa huduma ya afya ngazi ya jamii kuwafikia wananchi na kutoa elimu ya lishe kwa ufanisi zaidi.

Kikao hiki ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati mpana wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo katika kupambana na lishe duni na kuijenga jamii yenye afya bora, yenye uwezo wa kujifunza na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya Taifa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • SAMIA DAY: KATAVI YAANDAA TAMASHA KUBWA KUADHIMISHA MIAKA MITANO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA

    July 02, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE (LAAC)

    June 19, 2025
  • MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA WAZINDULIWA RASMI NSIMBO, MKOANI KATAVI

    June 09, 2025
  • KAMPENI YA MWEZI WA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    June 01, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa