• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

UZINDUZI WA KAMPENI YA UPANDAJI MITI 1,500,000 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO

Imewekwa: January 25th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mheshimiwa Filbert H. Sanga ameongoza kampeni ya upandaji miti katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo akiwa ni mgeni Rasmi katika uzinduzi wa kampeni hiyo katika chanzo cha Mto Ndurumo Kata ya Mtapenda Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo.

Katika uzinduzi huo Mheshimiwa Filbert H. Sanga  aliongoza zoezi la upandaji miti ambapo jumla ya miche 150 aina ya Mikuyu, ilipandwa katika chanzo cha mto Ndurumo ikiwa ni mkakati wa kuvitunza vyanzo vya maji, pia ikiwa ni mkakati kabambe wa Kitaifa wa kuhakikiksha kila Halmashauri inapanda miche 1,500,000 na kuisimamia kwa ukaribu.

Pamoja na uzinduzi huo katika chanzo cha maji Halmashauri imeweza kupanda miche 6169 katika kata 7 kati ya 12 zinazounda Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kuanzia tarehe 18/01/2023 mpaka leo tarehe 25/01/2023.

Tarehe 18/01/2023 Halmashauri ilipanda Miti katika Kata ya Sitalike pamoja na Kata ya Nsimbo. Katika Kata ya Nsimbo jumla miti 1,263 ilipandwa ikiwa miti 500 ilipandwa katika Shule ya Sekondari ya Anna Lupembe, miti 600 ilipandwa katika Shule ya Msingi Isanjandugu, Miti 100 katika Shule ya Msingi Tulieni na Miti 63 ilipandwa katika zahanati ya Isanjandugu. Pia katika kata ya Sitalike jumla ya miti 555 ilipandwa ikiwa miti 150 ilipandwa katika Shule ya Msingi Sitalike, 100 Shule ya Msingi Matandalani, 50 Shule ya Msingi Magula, 105 Shule ya Msingi Mtisi na 150 Shule ya Sekondari Sitalike.

Tarehe 19/01/2023 Halmashauri ilipanda Miti 950 katika Kata ya Mtapenda, kati ya miti hiyo miti 150 ilipandwa katika hospitali ya Wilaya ya Nsimbo, miti 300 ilipandwa katika Shule ya sekondari Mtapenda na miti 500 ilipandwa katika Shule ya Msingi Isinde.

Tarehe 20/01/2023 jumla ya miti 2533 ilipandwa katika kata za Itenka, Ibindi, Kapalala na Machimboni ikiwa ni katika Shule za Msingi, Shule za Sekondari, kituo cha Afya Itenka, ofisi za Kata na Makao makuu ya Halmasauri ya Wilaya ya Nsimbo.

Tarehe 24/01/2023 Miti 150 ilipandwa katika chanzo cha Mtapenda.

Idadi hiyo ya miche ya miti imejumulisha miche ya matunda (mipapai,mipera,matunda damu), Muarobaini, Mikangazi, Mikuyu (miche rafiki na Mazingira), Mijohoro, Jakaranda na Majani mapana (mbao).

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mhe. Halawa Charles Malendeja amewapongeza na kuwashukuru wadau pamoja na taasisi mbalimbali ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha malengo ya Upandaji miti kitaifa yanafikiwa katika Halmashauri yetu na Wilaya ya Mpanda kwa ujumla. Wadau pamoja na  taasisi hizo ni Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania – TFS wilaya ya Mpanda na Kanda ya Magharibi, Vyama vya Ushirika vya Katumba, Nsimbo na Ivungwe, Taasisi ya Jane Goodall na wananchi wote wa Halmashauri ya Nsimbo kwa ujumla wao na mwitikio wa upandaji miti.

“Tunza Mazingira tuing’arishe Nsimbo”

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa