• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

MAKARANI WAONGOZA WAPIGA KURA WAPEWA MAFUNZO - NSIMBO

Imewekwa: October 25th, 2025

Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais Wabunge na Madiwani unaotarajia kufanyika Jumatano ya Tarehe 29.10.2025, Makarani waongozaji wapiga kura katika vituo vya kupigia kura katika Jimbo la Nsimbo leo wamepewa mafunzo elekezi katika Jimbo la Nsimbo lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi.

Akifungua mafunzo hayo mapema hii leo, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Nsimbo Bwana Julius Z. Moshi amewasihi Makarani hao kuwa makini katika kipindi chote cha mafunzo yanayotolewa na watendaji wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, na hatimaye waweze kufuata taratibu, kanuni, sheria na miongozo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. “Ninyi mlioitwa kuja kupewa mafunzo hapa, mnapaswa kufuata taratibu, kanuni, sharia na miongozo na maelekezo yote yanayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi……..” ameongeza Bwana Moshi.

Bwana Julius Moshi amewasisitiza makarani hao kusoma katiba, sheria na miongozi inayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili kupata uelewa zaidi na na kuuliza kwa watu sahihi jambo lolote litakalohitaji ufafanuzi ili waendelee kutekeleza majukumu yao kwa weledi. Bwana Moshi amewataka makarani hao kufanya kazi kwa ushirikiano ili kurahisisha ufanyaji kazi kazi katika vituo vya kupigia kura. “fanyeni kazi kwa ushirikiano kama timu ili kurahisisha ufanyaji kazi kazi katika vituo vya kupigia kura…..” Amesema Bwana Moshi.

Makarani waongozaji wapiga kura wametakiwa kuzingatia unadhifu na kuwa na lugha ya staha kwa wapiga kura wote watakaofika katika kituo cha kupigia kura. “Hakikisheni mnazingatia unadhifu, lugha nzuri na kutoa kipaumbele kwa wapiga kura wenye mahitaji maalum wakapofika kituoni”

Aidha, baada ya mafunzo hayo, msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Nsimbo Bwana Julius Moshi amewapongeza wakufunzi pamoja washiriki wote wa mafunzo kwa uvumilivu, utulivu na umakini wao katika kipindi chote cha mafunzo. 

Bwana Moshi amewasihi washiriki wa mafunzo kutunza siri katika kipindi chote cha upigaji kura kama ambavyo wamekula kiapo chao cha kutunza siri. Bwana Moshi amesema ukikwaji wa kiapo walichokula ni makossa kwa mujibu wa sheria za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi   “washiriki wa mafunzo, kabla ya kuanza mafunzo mliapa kiapo cha kutunza siri, kipao hiki kipo kwa mujibu wa kanuni ya nane ya kanuni za uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani za mwaka 2025……”

 Katika mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku moja, jumla ya makarani 305 walihudhuria na kupewa mafunzo elekezi yatakayowaongoza kutekeleza majukumu yao katika jumla ya vituo 281 vitavyotumika katika upigaji kura katika Jimbo la Nsimbo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA MAKARANI NA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA NA KUITWA KUHUDHURIA MAFUNZO YA UCHAGUZI October 23, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MRADI WA KITUO CHA AFYA IBINDI August 26, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAKARANI WAONGOZA WAPIGA KURA WAPEWA MAFUNZO - NSIMBO

    October 25, 2025
  • MADAKTARI WA SAMIA - TUMAINI JIPYA LA AFYA KWA WANANCHI WA NSIMBO

    September 30, 2025
  • “MADAKTARI WA SAMIA” WATUA NSIMBO, MKURUGENZI AWAKARIBISHA WANANCHI KUCHUNGUZA AFYA ZAO

    September 27, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAKIMBIZWA NA KUKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO - NSIMBO DC

    September 25, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa