• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

ACHENI MILA POTOFU, FANYENI KAZI KWA WELEDI

Imewekwa: January 14th, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Eng. Stephano B. Kaliwa, amewataka viongozi wa serikali za vijiji kuacha mila potofu na kufanya kazi kwa weledi ili kuhakikisha utekelezaji wa miradi na shughuli za maendeleo unafanyika kwa ufanisi na kwa mujibu wa sheria. Akizungumza katika mafunzo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari Nsimbo kwa viongozi wa serikali za mitaa, yaliyojumuisha wajumbe wa serikali za Vijiji, wenyeviti wa Vitongoji, na maafisa watendaji wa Vijiji, Eng. Kaliwa alisisitiza umuhimu wa kuondokana na tamaduni zinazokwamisha maendeleo katika maeneo yao.

Mafunzo hayo yaliandaliwa na Chuo cha Serikali za Mitaa, Dodoma, yakilenga kuimarisha utawala bora na maendeleo endelevu katika ngazi za vijiji. Mafunzo hayo yalifunguliwa rasmi na Mkuu wa Chuo cha Serikali za Mitaa, ambaye alisisitiza umuhimu wa viongozi wa serikali za vijiji kuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko chanya kwa kufuata sheria na taratibu zilizopo.

Katika hotuba yake, Eng. Kaliwa ameonya dhidi ya vitendo vya kuua watu kwa tuhuma za uchawi, akisema kuwa tabia hizo hazikubaliki tena na zimepitwa na wakati. Amehimiza viongozi kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu ili kuleta maendeleo. Aidha, alibainisha kuwa viongozi wanapaswa kushirikiana kwa karibu ili kuhakikisha jamii inapata huduma bora. 

Kuhusu suala la usimamizi wa mihuri ya serikali za vijiji, amefafanua kuwa mihuri inapaswa kuwa chini ya afisa mtendaji wa kijiji badala ya mwenyekiti wa kijiji. Amesema kuwa hatua hiyo inalenga kudhibiti matumizi yasiyo halali ya mihuri na kuboresha utendaji wa serikali za vijiji. Hata hivyo, mabadiliko hayo yaliibua maswali kutoka kwa baadhi ya viongozi waliokuwa na mashaka kuhusu ufanisi wa mfumo huo. Eng. Kaliwa aliwataka viongozi kufuata miongozo ya waraka wa utekelezaji na kuacha mjadala usio wa lazima.

Kwa upande wake, Mhadhiri  Scholastica Nyabweke kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa, Dodoma, aliwahimiza viongozi wa serikali za vijiji kubuni vyanzo vipya vya mapato badala ya kutegemea tozo pekee. Alisema kuwa vyanzo hivyo vya mapato vitachangia kuongeza uchumi wa kijiji, vitongoji, na halmashauri kwa ujumla, huku akiwataka kuzingatia sheria, kanuni, na miongozo iliyotolewa na serikali.
Nyabweke ameleza kuwa changamoto kubwa inayowakabili viongozi wa vijiji ni ukosefu wa ufuatiliaji wa miradi na matumizi yasiyo ya uwazi ya rasilimali za umma. Alisema kuwa mafunzo hayo yataimarisha uwezo wa viongozi kusimamia rasilimali kwa uwazi na kushirikisha wananchi kikamilifu katika maendeleo. 

Mmoja wa wawezeshaji wa mafunzo hayo amesema kuwa lengo kuu la serikali ni kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora kuanzia ngazi za chini. Aidha, amebainisha kuwa mafunzo haya yanaweza kupunguza migogoro ya ardhi na changamoto nyingine zinazowakabili viongozi wa ngazi za chini.

Mafunzo haya, yaliyoandaliwana Chuo cha mafunzo ya uongozi cha serikali za mitaa Dodoma kwa ajili ya kuimarisha utawala bora na maendeleo endelevu, yameacha matumaini makubwa kwa washiriki. Viongozi walihitimisha kwa kuahidi kuzingatia mafunzo hayo ili kuleta mabadiliko chanya katika maeneo yao na kuhakikisha rasilimali za kijiji zinasimamiwa kwa maslahi ya jamii nzima. 

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE (LAAC)

    June 19, 2025
  • MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA WAZINDULIWA RASMI NSIMBO, MKOANI KATAVI

    June 09, 2025
  • KAMPENI YA MWEZI WA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    June 01, 2025
  • USHIRIKIANO WA JAMII NA VIONGOZI WA SERIKALI KUONDOA UDUMAVU NSIMBO

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa