• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

NSIMBO YAJIDHATITI KUSIMAMIA VIZURI MIRADI YA MAENDELEO - WAKANDARASI WAAGIZWA KUONGEZA KASI.

Imewekwa: December 4th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi imejidhatiti kikamilifu kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri hiyo kupitia vyanzo mbalimbali vya fedha.

Katika Halmashauri hiyo, Timu ya Ufuatiliaji na Tathmini (M&E) imeendelea na ukaguzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo mbalimbali katika Halmashauri hiyo. Timu hiyo iliyoongozwa na Mkuu wa idara ya mipango Bwana Mohamed Hussein, pamoja na miradi mingine, imekagua miradi ya afya na elimu.

Katika Kata ya Ugalla, timu hiyo imekagua mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Kalele ambapo ujenzi umefikia katika hatua ya ukamilishaji. Katika hatua hiyo ya ukamilishaji, mradi huo ulitengewa kiasi cha shilingi milioni 35 ambapo tayari vifaa vimefika katika eneo hilo tayari kuanza kazi. Aidha, baadhi ya wazabuni walioshinda tenda ya kupeleka vifaa na bado havijafika katika eneo la mradi wamepewa siku tatu kuhakikisha vifaa vyote vimefika.

Aidha, katika mradi wa ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi katika Kijiji cha Katambike, mradi huo unaendelea na ujenzi uko katika hatua ya kunyanyua kuta kwa baadhi ya majengo. Ujenzi huo unaoendelea uko nyuma ya muda kutokana na uchache wa mafundi katika eneo la mradi. Ambapo mkandarasi ameagizwa kuongeza idadi ya mafundi ili mradi huo uwe umekamilika ifikapo disemba 23 mwaka huu kwa mujibu wa mkataba.  

Bwana Mohamed Hussein amemuagiza mhandisi kusimamia vizuri mradi huo ili ukamilike kwa haraka. 

“engineer simamia tarehe 23 majengo haya yakamilike, wakupe mpango kazi wa mpaka tarehe 23…”  

Katika mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Lukama unaotekelezwa katika Kata ya Litapunga, mradi huo uko katika hatua ya upauaji ambapo tayari kazi ya kuezeka bati imekamilika na mafundi wanaendelea na shughulo zingine za ukamilishaji wa mradi huo.

Mradi wa ujenzi wa Zahanati hiyo ulioanzishwa kwa nguvu za wananchi ulipewa kiasi cha shilingi milioni 65 katika hatua za ukamilishaji wake.

Pamoja na miradi mingine timu hiyo ya ufuatiliaji na Tathmini imesisitiza mafundi kuongeza kasi ya ujenzi ili miradi yote ikamilike kwa wakati.



Matangazo

  • UCHAGUZI WA KIDATO CHA KWANZA 2026 December 04, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MRADI WA KITUO CHA AFYA IBINDI August 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA November 13, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • NSIMBO YAJIDHATITI KUSIMAMIA VIZURI MIRADI YA MAENDELEO - WAKANDARASI WAAGIZWA KUONGEZA KASI.

    December 04, 2025
  • DED NSIMBO AWAALIKA WANANCHI KUHUDHURIA MKUTANO WA KWANZA WA BARAZA LA MADIWANI.

    December 01, 2025
  • NSIMBO YAENDELEA KUTEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

    November 28, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA MPANDA AHIMIZA UPANDAJI MITI, ASISITIZA AMANI NCHINI

    November 26, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa