• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA NSIMBO LAFANYA KIKAO CHA KAMATI KUWASILISHA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI ROBO YA PILI 2025/2026

Imewekwa: January 22nd, 2026

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, mkoani Katavi, limefanya kikao chake cha pili katika ukumbi mdogo wa Halmashauri hiyo, ambapo wajumbe walijadili ajenda mbalimbali zilizowasilishwa na kamati za kudumu za Baraza hilo.

Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Mheshimiwa Athumani Juma Fimbo, kwa kushirikiana na Katibu wa Baraza ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Bi. Christina Bunini. Kikao hicho kilifanyika kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizopo.

Katika kikao hicho, kamati mbalimbali za kudumu ziliwasilisha taarifa zao za kiutendaji kwa kipindi cha Oktoba hadi Desemba, 2025. Kamati hizo ni pamoja na Kamati ya Kudhibiti Ukimwi, Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira, Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, Kamati ya Maadili, pamoja na Kamati ya Elimu, Afya na Maji.

Akijibu hoja kutoka kwa wajumbe wa Kamati ya Elimu, Afya na Maji, Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Bw. Elisenguo Mshiru, alieleza kuwa wanafunzi wa kidato cha kwanza bado wanaendelea kuripoti shuleni. Aliongeza kuwa zoezi la uhamasishaji linaendelea kwa kuwahimiza wazazi na walezi wa watoto waliopata nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza kuhakikisha wanaripoti mapema ili kuanza masomo mara moja.

Aidha, Baraza hilo liliaridhia uthibitisho wa watumishi wawili waliokuwa wakikaimu katika nafasi zao, na kuthibitishwa rasmi kuwa wakuu wa idara. Watumishi hao ni Bi. Bertha Ng’eve, aliyethibitishwa kuwa Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, pamoja na Bw. Petro Mwita aliyethibitishwa kuwa Mkuu wa Idara ya Miundombinu na Maendeleo ya Vijijini na Mijini.

Miongoni mwa wageni waalikwa waliohudhuria kikao hicho ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mpanda, Ndugu Joseph Anniseth Lwamba, Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Mheshimiwa Jamila Yusuph Kimaro, Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpanda, Ndugu Juma A. Njeru, pamoja na wageni wengine kutoka Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Mpanda.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA UKUSANYAJI WA MAPATO February 02, 2026
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MRADI WA KITUO CHA AFYA IBINDI August 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA November 13, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAKIKISHEN MNAWAWEZESHA VIJANA KIUCHUMI-DC MPANDA

    January 22, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA NSIMBO LAFANYA KIKAO CHA KAMATI KUWASILISHA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI ROBO YA PILI 2025/2026

    January 22, 2026
  • HALMASHAURI YA NSIMBO YAPELEKA NEEMA KWA WAFANYABIASHARA, WANANCHI KIJIJI CHA MAGULA

    January 22, 2026
  • RC MRINDOKO AHIMIZA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO – NSIMBO DC

    December 17, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa