• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

HAKIKISHEN MNAWAWEZESHA VIJANA KIUCHUMI-DC MPANDA

Imewekwa: January 22nd, 2026

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Mheshimiwa Jamila Yusuph, amewataka viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo mkoani Katavi kuhakikisha wanawawezesha vijana kwa kuwapatia mikopo itakayowasaidia kujikwamua kiuchumi.

Mheshimiwa Jamila ameyasema hayo Januari 22, 2026, alipokuwa akizungumza katika Kikao cha Pili cha Baraza la Madiwani kilichofanyika katika ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo. Ambapo amewataka Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mheshimiwa Juma Fimbo, pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bi Christina D. Bunini kuhakikisha kuwa makundi ya vijana na wanawake yanapewa kipaumbele katika utoaji wa mikopo ya asilimia kumi inayotolewa ndani ya halmashauri hiyo.

“Wapo vijana ambao tayari wana miradi inayoendelea, lakini wameomba kuwezeshwa zaidi ili kukuza shughuli zao na hatimaye kuweza kuwaajiri vijana wenzao. Imani yangu ni kwamba maombi hayo yatafanyiwa kazi na watapewa kipaumbele katika kupatiwa mikopo hiyo” alisema Mheshimiwa Jamila.

Aidha, Mheshimiwa Jamila amewataka viongozi wa halmashauri hiyo kuhakikisha kuwa utoaji wa mikopo unaambatana na elimu ya ujasiriamali, ikiwemo namna ya kutambua fursa za kiuchumi zilizopo ndani ya halmashauri hiyo na mbinu bora za uendeshaji wa biashara ili kuhakikisha kuwa wanapata faida katika miradi yao na kurejesha mikopo kwa wakati.

Kwa upande mwingine, Mheshimiwa Jamila ameiagiza Kamati ya Fedha ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kufanya ufuatiliaji na ukaguzi wa mara kwa mara kwa vikundi vilivyonufaika na mikopo hiyo, kwa lengo la kutathmini maendeleo ya miradi yao na kuwasaidia kutatua changamoto wanazokumbana nazo, ili kufikia lengo kuu la mikopo hiyo ambalo ni kuwawezesha wananchi kujikwamua kiuchumi na kukuza maendeleo ya halmashauri pamoja na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA UKUSANYAJI WA MAPATO February 02, 2026
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MRADI WA KITUO CHA AFYA IBINDI August 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA November 13, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAKIKISHEN MNAWAWEZESHA VIJANA KIUCHUMI-DC MPANDA

    January 22, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA NSIMBO LAFANYA KIKAO CHA KAMATI KUWASILISHA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI ROBO YA PILI 2025/2026

    January 22, 2026
  • HALMASHAURI YA NSIMBO YAPELEKA NEEMA KWA WAFANYABIASHARA, WANANCHI KIJIJI CHA MAGULA

    January 22, 2026
  • RC MRINDOKO AHIMIZA USIMAMIZI MZURI WA MIRADI YA MAENDELEO – NSIMBO DC

    December 17, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa