• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Bil 2.55 za mapambano ya UVIKO 19, Mwenyekiti,DED Nsimbo wamshukuru Rais Samia.

Imewekwa: October 27th, 2021

Na: John Mganga-IO Nsimbo DC

Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo imeidhinishiwa kupokea kiasi cha Shilingi 2,550,000,000.00 kwa ajili ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo kwa ustawi wa taifa na mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19 ambapo  fedha hizo zimeelekezwa kwenye maeneo ya vipaumbele vinavyogusa Wananchi moja kwa moja kwa ajili ya kuwaondolea kero katika kuzifikia huduma za Elimu na Afya.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mh.Halawa Charles Malendeja pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mohamed Ramadhani wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan kwa jitihada mbalimbali anazofanya katika kufufua uchumi kwa sekta zilizopata athari za kiuchumi kutokana na madhara ya UVIKO 19.

Katika Taarifa yake mbele ya kikao cha  Baraza la Madiwani la  Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kilichoketi 21 Oktoba 2021,Mkuu wa Idara ya Mipango Takwimu na Ufuatiliaji Nsimbo Viktoria Cilewa ameeleza kuwa kati ya fedha hizo zilizotolewa,Shilingi 860,000,000.00 zitatumika kwa ajili ya Ujenzi wa Vyumba 43 vya madarasa kwa ajili ya kujiandaa  kupokea Wanafunzi wa kidato cha kwanza watakaojiunga Mwezi Januari 2022 ambapo ujenzi huo utajumuisha pia utengenezaji wa viti na meza 2150 na kwamba Idadi ya vyumba vya madarasa utatofautiana kutoka shule moja hadi nyingine  kulingana na mahitaji.

Amezitaja Shule za Sekondari Nsimbo zitakazonufaika na Fedha hizo kuwa ni  Shule ya Sekondari ya   Itenka,Ivungwe,Kanoge,Katumba,Kenswa,Kaboronge,Mtapenda,Nsimbo,Sitalike,Ugalla River,Uruwira pamoja na Shule ya Sekondari ya Machimboni ambazo kila moja itapokea fedha hizo kulingana na mahitaji yaliyopo.

Kwa upande wa Elimu msingi kiasi cha Shilingi 880,000,000.00 kimeelekezwa kwa ajili ya Ujenzi wa Vyumba 44 vya madarasa katika vituo shikizi 11 ambavyo hutumika kwa ajili ya kufundishia Wanafunzi wa Awali hadi darasa la tatu wanaokaa mbali na Shule mama ambapo imeelezwa kuwa hatua hiyo, itapunguza adha ya umbali kwa Wanafunzi 1980 na hivyo kupunguza kuondoa kabisa tatizo la   utoro ambapo pia ameeleza kuwa ujenzi huo utaendana na utengenezaji wa madawati 660 ambapo kila chumba kitakuwa na madawati 15.

Amevitaja vituo shikizi vitakavyonuifaika na fedha hizo kuwa ni Motomoto,Kalele,Kamini,Kazaroho,Sikwisi,Mtambo B,Tulieni,Imilamate,Jilabela,na kituo Shikizi cha Magula ambapo kila kimoja kitapatiwa kiasi cha Shilingi Mil.20

Akizungumzia kuhusu Sekta ya Afya Afisa Mipango Nsimbo ameeleza kuwa Kiasi cha Shilingi Milioni 810,000,000.00 zimeelekezwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya Afya Nsimbo ambapo kati ya hizo Shilingi 300,000,000.00 zitatumika kwa ajili ya Ujenzi wa Jengo la huduma ya dharura(EMD) katika Hospitali ya Halmashauri .Aidha Shilingi Milioni 420,000,000.00 zitatumika kwa ajili ya ununuzi wa Jengo la X-RAY,pamoja na Shilingi Mil 90,000,000.00 zilizobaki zimeelekezwa kwenye Ujenzi wa Nyumba vya Watumishi  kwa vituo vilivyoko mbali na Makao makuu.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa