• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

DED awashukia Watendaji Nsimbo, Awataka kuacha Visingizio,kukamiilisha miradi ndani ya muda uliopangwa.

Imewekwa: April 21st, 2022

Pichani:(Katikati)Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw Mohamed Ramadhani alipozungumza na walimu wakuu,wakuu wa Shule,Wafawidhi wa Vituo,Wakuu wa Idara na Vitengo,pamoja na Watendaji wa Kata wenye Miradi(Hawako pichani) katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Nsimbo 20, Aprili 2022.

Nsimbo-Mtapenda.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Mohamed Ramadhani amewataka Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wanaosimamia miradi mbalimbali ya Ujenzi inayotekelezwa ndani ya mwaka wa fedha 2021/2022 kuacha visingizio na badala yake wahakikishe wanakamilisha miradi hiyo ndani ya muda uliopangwa.

Mkurugenzi Mohamed ametoa  rai hiyo Katika kikao na Wakuu wa Shule,Walimu wakuu,Wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za Afya,Watendaji wa Kata wenye miradi pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Nsimbo 20, Aprii 2022.

Amebainisha kuwa kutokamilika kwa miradi ndani ya muda uliopangwa kunasababishwa na baadhi ya Watendaji kutowajibika ipasavyo katika nafasi zao hali inayopelekea miradi mingi ya Serikali kuchelewa kukamilika wakati.

Amewasisitiza watendaji hao kuhakikisha kuwa wanatoa taarifa kwa  wakati  pindi wanapopatwa na chamgamoto kwa kuwa kufanya hivyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuchukuliwa hatua madhubuti kutatua changamoto katika eneo husika kwa haraka zaidi.

Aidha Mkurugenzi Mohamed ameongeza kuwa tabia ya Baadhi ya Watendaji kutokuwa waaminifu na kutanguliza maslahi binafsi mbele nayo kwa sehemu kubwa inachangia kuzorotesha utekelezaji wa miradi Serikalini.

Kutokana na sababu hizo Mkurugenzi Mohamed amewaagiza Watendaji hao kuacha visingizio na badala yake kila mmoja awajibike ipasavyo katika nafasi yake ili kuhakikisha kuwa miradi yote iliyotengewa na kupewa fedha kukamilika mapema kabla ya Tarehe 30 Juni 2022.

Ameeleza kuwa endapo Watumishi wa Serikali watatekeleza majukumu yao kwa Uadilifu na bidii pamoja na kutanguliza maslahi mapana ya Taifa mbele itasadia kwa kiasi kikubwa kukamilika kwa miradi mbalimbali ya maendeeo ndani ya muda uliopangwa jambo litakaloharakisha maendeleo.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi Mohamed amewataka Watumishi hao kuepuka kufanya urasimu usiokuwa na lazima kwa kuwa kufanya hivyo kwa sehemu kubwa ndiko kunakoathiri utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo na hivyo kupelekea kutokamilika kwa miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa wakati.

Ametoa wito kwa Watalaamu hao kuhakikisha kuwa wanafanya maandalizi ya manunuzi ya Vifaa vya Ujenzi kwa wakati pamoja na kujiridhisha na ubora wakati wa manunuzi ili kuepuka kuleta sintofahamu zinazojitokeza wakati wa ukaguzi wa miradi hiyo.

Kwa Upande wao Walimu wakuu,Wakuu wa Shule pamoja na Watendaji wa Kata wenye miradi  Nsimbo, wametaja sababu ya miradi kuchelewa kukamilika kuwa ni pamoja na baadhi ya mafundi wanaopewa kazi za Ujenzi kuzidiwa na  kazi nyingi hali inayosababishwa na uhaba wa Mafundi Nsimbo.

Aidha wameitaja changamoto ya umbali kuwa sababu kubwa inayoathiri ukamilisha wa miradi kutokana na malighafi pamoja na vifaa vya Ujenzi kuwa mbali na eneo la Ujenzi huku wakitaja hangamoto ya Usafiri kuathiri Utekelezaji wa Miradi hiyo ya Ujenzi.

Matangazo

  • MAFUNZO YA SENSA KWA WALIOCHAGULIWA KWENYE KAZI YA MUDA YA TEHAMA, UKARANI NA USIMAMIZI WA SENSA July 28, 2022
  • ORODHA YA WALIOCHAGULIWA KWENYE KAZI YA MUDA YA UKARANI NA USIMAMIZI WA SENSA July 28, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI July 26, 2022
  • MAELEKEZO YA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO,SHULE YA SEKONDARI NSIMBO MWAKA WA MASOMO 2022/2023 April 08, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • UZINDUZI WA KAMPENI YA UPANDAJI MITI 1,500,000 KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO

    January 25, 2023
  • MILIONI MIA MOJA NA TISA ZATOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU KATIKA MWAKA WA FEDHA 2021/2022

    June 29, 2022
  • Kamati za Sensa za Vitongoji, Vijiji na Kata Nsimbo wajengewa uwezo wa kutekeleza majukumu yao

    May 27, 2022
  • DED awashukia Watendaji Nsimbo, Awataka kuacha Visingizio,kukamiilisha miradi ndani ya muda uliopangwa.

    April 21, 2022
  • Angalia zote

Video

ZIara ya Naibu Waziri OR TAMISEMI Mh.David Silinde kukagua Ujenzi wa Madarasa Nsimbo DC
Video zaidi

Quick Links

  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa
  • Orodha ya waheshimiwa madiwani
  • Sheria ndogo za Halmashauri
  • Video mbalimbali
  • Muundo wa Halmashauri
  • Picha mbalimbali
  • Fomu mbalimbali

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa