• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

ELIMU YA LISHE IWAFIKIE WANANCHI

Imewekwa: October 22nd, 2024

Mkurugenzi Mtendaji Eng. Stephano B. Kaliwa aliwataka wajumbe kuhakikisha wanazingatia elimu inayotolewa juu ya lishe bora kwa maendeleo ya jamii.  Aliyasema hayo wakati akifungua kikao muhimu cha Afya na Lishe, kilichofanyika kama sehemu ya vikao vya utekelezaji wa afua za lishe ya robo ya kwanza katika mwaka wa fedha 2024/2025.Kikao hicho kilifanyika kwa lengo la kutathmini na kujadili masuala ya afya na lishe ndani ya halmashauri.

Katika hotuba yake Mkurugenzi Mtendaji Alisisitiza kuwa ni muhimu kwa wananchi kutumia mbinu za lishe bora ili kupunguza magonjwa yanayotokana na lishe duni, hasa kwa makundi maalum kama watoto, wajawazito na wazee

Afisa Lishe, akitoa mchango wake, alielezea hatua mbalimbali ambazo Halmashauri imechukua katika kuhakikisha kuwa elimu ya lishe inawafikia wananchi kwa ufanisi. Pia alitoa ushauri wa kitaalamu juu ya vyakula vinavyohitajika kuboresha lishe na kuimarisha afya. Alisisitiza kuwa lishe bora ni msingi wa jamii yenye afya njema na tija.

Wajumbe wa kikao hicho walipata fursa ya kuchangia maoni yao, ambapo walijadili mafanikio na changamoto zinazowakabili katika utekelezaji wa mpango wa afya na lishe. Baadhi walipendekeza mbinu za kuongeza ufanisi wa utoaji elimu ya lishe na afya kwa wananchi ili kuhakikisha wanapata uelewa mpana juu ya masuala hayo muhimu.

Mwenyekiti wa kikao, Mkurugenzi Mtendaji ,alihitimisha kwa kutoa wito kwa wote waliohudhuria kuhakikisha wanatekeleza kwa vitendo mapendekezo yaliyotolewa na wataalamu wa lishe. Alisema kuwa ushirikiano wa wananchi na wataalamu ni muhimu katika kufikia malengo ya afya bora na lishe katika Halmashauri ya Nsimbo.

 Aidha,amesema kuwa elimu ya lishe pamoja na kutolewa shuleni bado ni muhimu kutolewa majumbani pamoja na vituo vya afya. Aliwataka madaktari na wadau wote wa afya kuhakikisha kuwa afya inachukuliwa kama agenda kuu na utekelezaji wake ufanyike haraka wakati wote bila kutoa sababu ambazo hazilingani na umuhimu wake.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa