• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE (LAAC)

Imewekwa: June 19th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Bw. Albert Msovela, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kwa utekelezaji madhubuti wa maagizo ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), ikiwa ni sehemu ya majibu ya hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024

Pongezi hizo zilitolewa leo katika Baraza la Hoja la Halmashauri ya Nsimbo lililofanyika katika Ukumbi Mdogo wa Halmashauri, ambapo Bw. Msovela alihudhuria kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Katika hotuba yake, Katibu Tawala alieleza kuwa madiwani wa Halmashauri ya Nsimbo wamekuwa sehemu muhimu ya mafanikio kutokana na ushirikiano wao wa karibu na wataalamu wa Halmashauri katika kutekeleza maagizo ya LAAC pamoja na kusimamia miradi ya maendeleo kwa ufanisi. Aidha, alimpongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Bi. Christina Daniel Bunini, kwa uongozi wake wa kijasiri na kitaalamu. Alisema kuwa nidhamu ya kiutendaji inayojengwa kupitia usikivu wake ni msingi imara wa mafanikio ya Halmashauri hiyo. 

Akizungumza mbele ya wajumbe wa Baraza la Madiwani, Bw. Msovela alisema kuwa Halmashauri ya Nsimbo imekuwa mfano wa kuigwa kwa kujibu na kutekeleza maagizo kwa weledi na kwa wakati, hatua inayoonesha uwajibikaji na uzingatiaji wa misingi ya utawala bora. “Pamoja na kuwepo kwa hoja, hatua zilizochukuliwa zinaonyesha dhamira ya dhati ya Halmashauri hii kuleta mabadiliko. Kama majibu yangewasilishwa kwa wakati na kwa vielelezo kamili, hoja nyingi zingeweza kuepukwa,” alisema.

Aliwataka watumishi waendelee kuzingatia sheria, taratibu na miongozo ya kazi ili kuhakikisha hoja zote zilizobaki zinapatiwa majibu sahihi kwa wakati. 

Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa na Mkaguzi wa Ndani, Bw. Chambi Ngelela, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo imepokea hati ya kuridhisha (Unqualified Opinion) kutoka kwa CAG. Ripoti hiyo imeonesha kuwa hoja 19 kati ya zilizowasilishwa zimefungwa, huku hoja 40 bado hazijafungwa, huku maagizo yote 6 ya LAAC yakiwa yametekelezwa.

Akihitimisha kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, Mhe. Halawa Charles Malendeja, kwaniaba ya Madiwani wote, alieleza kuwa mafanikio haya yametokana na mshikamano wa kweli kati ya wataalamu wa Halmashauri na viongozi wa kisiasa. Ushirikiano huo umewezesha utekelezaji mzuri wa mipango ya maendeleo na majukumu ya kiutawala kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI BORA WA MAAGIZO YA KAMATI YA BUNGE (LAAC)

    June 19, 2025
  • MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA WAZINDULIWA RASMI NSIMBO, MKOANI KATAVI

    June 09, 2025
  • KAMPENI YA MWEZI WA AFYA NA LISHE YA MTOTO

    June 01, 2025
  • USHIRIKIANO WA JAMII NA VIONGOZI WA SERIKALI KUONDOA UDUMAVU NSIMBO

    May 30, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa