Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi imejidhatiti kutoa hudumu zote muhimu za afya hasa baada ya kukamilika kwa miundombinu mbalimbali na muhimu inayowezesha utoaji wa huduma za afya.
Hayo yamebainishwa hivi karibuni na mganga mfawidhi wa Hospitali hiyo Dkt Patrick Tulyanje wakati akifanya mahojiano maalum na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo.
Dkt. Tulyanje amezitaja baadhi ya huduma zinazotolewa katika Hospitali hiyo ni pamoja na huduma ya wagonjwa wa nje (OPD), huduma ya dharura, maabara, mionzi, huduma kwa mama na mtoto, RCH, huduma ya kuhifadhi maiti (Mortuary) pamoja na huduma zingine mihimu.
Hivi karibuni kwa mara ya kwanza hospitali hiyo imefanikiwa kutoa huduma ya upasuaji wa dharura kwa wanawake wawili wajawazito waliopata changamoto za kujifungua kwa njia ya kawaida na kutekeleza huduma hiyo kwa ufanisi wa hali ya juu.
Kwa upande wao, baadhi ya wananchi waliofika kupata huduma za afya katika Hospiatali hiyo wameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayooongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha huduma ya afya inapatikana katika maeneo yao, huku wakiipongeza huduma nzuri inayotolewa na wahudumu wa afya katika Hospitali hiyo. Bi. Delphina Mshanga na Bw. Peter Hoja ni mingoni mwa wananchi walipata wasaa wa kuzungumza nasi.
“Kiukweli tunaishukuru sana serikali kwa kutusogezea huduma ya afya karibu kwasababu isingekuwa hii tungekuwa tunapata changamoto kubwa sana, tungekuwa tunasafiri umbali mrefu kwenda kufuata huduma kama hii………” Amesema Bi. Delphina Mshanga, mmoja wa wananchi waliofika Hospitalini hapo kupata huduma ya afya.
Bw. Peter Hoja amesema anaishukuru serikali kwakuwa inafanya kazi nzuri sana katika utoaji wa huduma kwa wananchi huku akiwashukuru wahudumu kwa mapokezi mazuri na huduma nzuri alizopatiwa ndugu yake tangu alipofika Hospitalini hapo.
“mpaka sasa hivi naishukuru sana hii serikali, serikali imefanya kazi nzuri ya kutuletea huduma ……….” Amesema bwa Peter Hoja
Mpanda to Tabora road
Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda
Simu : 025 295 5164
Simu: 025 295 5164
Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz
Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa