• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

HOSPITALI YA WILAYA YA NSIMBO YATOA HUDUMA YA UPASUAJI KWA MARA YA KWANZA

Imewekwa: February 12th, 2026

Hospitali ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi kwa mara ya kwanza imefanikiwa kutoa huduma ya upasuaji kwa wanawake waliofika Hospitalini hapo kwa lengo la kupata huduma ya uzazi.

Kupitia uboreshaji wa miundombinu iliyofanyika katika sekta ya afya, Hospitali hiyo imefanikiwa kutoa huduma ya upasuaji kwa wanawake wawili waliofika kupata huduma ya uzazi tarehe 12 February 2026 baada ya kupewa rufaa kutoka kituo cha afya Katumba.

Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Nsimbo Dkt. Patrick Tulyanje amesema Madaktari na wauguzi walifanikiwa kuwapatia huduma ya dharua ya kuijifungua kwa njia ya upasuaji wajawazito wawili waliofika kupata huduma ya kujifungua. Dkt. Tulyanje amesema upasuaji ulifanyika salama na wote walitoka salama na wazazi hao wanaendelea vizuri pamoja na watoto wao wakiwa na afya njema.

“wamama hao wote wawili walifanyiwa operesheni na madkatari pamoja na wauguzi katika hospitali yetu kwa mara ya kwanza na tukafanikiwa kutoka salama mpaka sasa hivi wanaendelea vizuri akina mama pamoja na watoto wao………”  amesema Dkt. Tulyanje.

Aidha, Dkt. Tulyanje ameishukuru serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha huduma ya afya na kuwapatia fedha za ukamilishaji wa miundombinu katika Hospitali hiyo.

“kimsingi tunamshukuru Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha za kukamilisha miundombinu, kutupatia vifaa tiba ambapo mpaka leo tumefanikiwa kuokoa maisha ya hao akina mama wajawazito na tutaendelea kutoa huduma ya namna hiyo……………….” Ameongeza Dkt Tulyanje. 

Kwa upande wao, wanawake waliopatiwa huduma ya upasuaji katika Hospitali hiyo wameishukuru serikali kwa kuboresha huduma za afya katika maeneo yao jambo linalorahisisha upatikanaji wa huduma karibu nao wakatim wowote. Bi. Shamsia Salehe amesema ameridhishwa na huduma iliyotolewa na wahudumu wa afya katika hospitali hiyo kwakuwa alihudumiwa haraka.

“jopo la wauguzi waliofika tu kwanza walinifurahisha kwasababu walikuwa wakarimu, wachangamfu, huduma zilienda kwa wakati, muda huo huo saa tisa niliingizwa theatre kunifanyia operesheni, operesheni ilienda vizuri kwakweli nili enjoy, sijasikia maumivu ya aina yoyote……….”  Ameongeza Bi. Shamsia Salehe.

Pamoja naye, Bi. Loveness Donasiano amesema kuwa amefurahishwa na uchangamfu wa wahudumu kwakuwa walijitoa haraka kuokoa maisha yao jambo lililomfanya ampe mwanae jina la Daktari aliyemhudumia.  

“kwa jinsi walivyonifanyia vizuri wakanihudumia vizuri nimeamua kumwita jina la mhudumu aliyenihudumia anaitwa David……..”  amesema Bi. Loveness Donasiano.

 Huduma ya kujifungua kwa njia ya upasuaji imekuwa ya kwanza katika Hospitali ya Wilaya ya Nsimbo tangu ilipoanza kutoa huduma za afya, jambo linalorahisisha upatikanaji wa huduma za afya karibu na wananchi wa Nsimbo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI YA UKUSANYAJI WA MAPATO February 02, 2026
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MRADI WA KITUO CHA AFYA IBINDI August 26, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA November 13, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HOSPITALI YA WILAYA YA NSIMBO YATOA HUDUMA YA UPASUAJI KWA MARA YA KWANZA

    February 12, 2026
  • ZOEZI LA UHAKIKI NA UGAWAJI KADI ZA BIMA YA AFYA LAANZA RASMI NSIMBO

    February 06, 2026
  • HAKIKISHEN MNAWAWEZESHA VIJANA KIUCHUMI-DC MPANDA

    January 22, 2026
  • BARAZA LA MADIWANI HALMASHAURI YA NSIMBO LAFANYA KIKAO CHA KAMATI KUWASILISHA TAARIFA ZA UTEKELEZAJI ROBO YA PILI 2025/2026

    January 22, 2026
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa