• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

Imewekwa: April 29th, 2025

Kamishna wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bi. Asina Omari, Atembelea mafunzo ya Waandikishaji Wasaidizi na Waendesha Vifaa vya Kielektroniki vya Bayometriki (BVR Kits) katika Jimbo la Nsimbo, ambapo alisisitiza umuhimu wa uadilifu, weledi, na uzingatiaji wa sheria katika utekelezaji wa majukumu ya uandikishaji wa wapiga kura kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Akizungumza katika mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Nsimbo, Kamishna Asina alisema kuwa mabadiliko yoyote yanayofanyika katika mfumo wa uandikishaji yanahitaji umakini mkubwa. Alieleza kuwa kila hatua ya mchakato huo inapaswa kutekelezwa kwa usahihi na uaminifu ili kuhakikisha kila mwananchi anapata haki yake ya kikatiba ya kupiga kura bila vikwazo vya kiutendaji.

“Elimu mliyoipata ni dira itakayowaongoza kutekeleza kazi zenu kwa vitendo. Hakikisheni mnafuata mwongozo wa Tume kwa umakini na kutimiza majukumu kwa uadilifu,” alisema Kamishna huyo.

Amesisitiza kuwa washiriki wanapaswa kutekeleza majukumu yao kwa ushirikiano, kwa kuzingatia sheria, taratibu na viapo vya uaminifu walivyoweka mbele ya Tume, kama ishara ya dhamira ya kufanya kazi kwa uwazi na ufanisi. Aliongeza kuwa ubora wa kazi yao ndio msingi wa kuaminika kwa mchakato mzima wa uchaguzi.

Kwa upande wake, Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Nsimbo, Bw. Adolf Issaya Semindu, alisema kuwa washiriki wamepewa maarifa ya matumizi sahihi ya vifaa vya uandikishaji, ujazaji wa fomu rasmi, utunzaji wa vifaa kama mashine za BVR, daftari la wapiga kura, na kudumisha usiri wa taarifa hadi pale taratibu rasmi zitakapokamilika.

“Watendaji hawa sasa wana uelewa wa nadharia na vitendo kuhusu zoezi la uandikishaji. Ni wajibu wao kuhakikisha wanatekeleza majukumu kwa weledi kwa mujibu wa sheria, kanuni na miongozo ya Tume,” alisema Bw. Semindu.

Mafunzo hayo yamehitimishwa kwa viapo vya uaminifu kutoka kwa Waandikishaji Wasaidizi, waliokiri kwa dhati kuwa watatekeleza majukumu yao kwa uwajibikaji na uadilifu wa hali ya juu. Washiriki pia walipata fursa ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi wa kina ili kuondoa mkanganyiko kabla ya kuanza kwa zoezi lenyewe.

Mafunzo haya ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kuhakikisha kuwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 unaendeshwa kwa uwazi, usalama na haki kwa wananchi wote.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa