• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

MAONYESHO YA WIKI YA MWANAKATAVI YATAKIWA KUWA YA KIMATAIFA

Imewekwa: October 25th, 2024

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mh. Mwanamvua Hoza Mrindoko amesisitiza umuhimu wa kuwapa wafanyabiashara wadogo nafasi na kuhakikisha kwamba wanapewa mabanda katika eneo la maonyesho ili waweze kuonyesha na kujitangaza katika biashara ama shughuli za kiuchumi wanazofanya. Alisema kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameonyesha jitihada zake za kuleta maendeleo ambayo yameonekana kusaidia sekta mbalimbali, ikiwemo biashara na ujasiriamali. Alisema hayo wakati akifungua rasmi maonyesho ya wiki ya mwanakatavi yanayoendelea kufanyika katika uwanja wa Azimio Manispaa  Mpanda hadi ifikapo tarehe 31/10/2024 ambapo ni kilele cha maonyesho haya.

Katika hotuba yake, Mkuu wa Mkoa amesema kuwa wiki  ya Mwanakatavi inafanyika  kwa mafanikio makubwa, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kukuza uchumi na kutoa fursa kwa wafanyabiashara wakubwa na wadogo kuonyesha bidhaa na huduma zao.  Alieleza kuwa haya ni maonyesho yaliyobeba matukio mengi yenye manufaa makubwa na yanayolenga kuitangaza Tanzania kwa ujumla. Amesema huduma sasa zimesogezwa karibu hivyo wananchi wajitokeze ili kupata huduma.

Aidha, amesema kuwa Maonyesho hayo yaliyoandaliwa kwa umakini yamewezesha wadau kuweka mabanda mbalimbali ambapo biashara na shughuli zote zimewekwa wazi kwa wananchi na wageni waliofika kwa wingi. Halmashauri zote za mkoa wa Katavi zilikuwa banda kwa ajili ya kuonyesha shughuli zake.

Vivyohivyo, Mkuu wa Mkoa alipata wasaa wa kutembelea mabanda mbalimbali likiwemo banda la Halmashauri ya Nsimbo ambalo lilikuwa limesheheni shughuli mbalimbali za kiuchumi na bidhaa nyingi za kilimo pamoja na lishe bora. Mkuu wa mkoa alifurahishwa na kuwepo kwa banda maalumu la kusikiliza kero za wananchi. Aliwataka wananchi kujitokeza ili kuwasilisha kero zao kwani Serikali ya Mama Samia ni sikivu na wote watahudumiwa kwa karibu.

Akiendelea kuhutubia katika ufunguzi wa maonyesho hayo, alitoa agizo kuwa mwaka ujao maonyesho ya wiki ya Mwanakatavi yanapaswa kufikia kiwango cha kimataifa. Lengo likiwa ni kuvutia wawekezaji na wafanyabiashara kutoka mataifa mbalimbali. Alieleza kuwa Mkoa wa Katavi ni moja kati ya mikoa yenye vivutio vingi vya kuwavutia wageni hivyo itakuwa ni fursa ya kupata ongezeko la kiuchumi.

Katika ufunguzi wa maonyesho haya  viongozi wa Serikali na Chama walihudhuria  ambapo  Mkuu wa Wilaya na viongozi wengine walitoa hotuba zenye kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika maonyesho haya na kukuza ushirikiano kati ya sekta za umma na binafsi.

 Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh. Jamila Yusuph Kimaro aliwahimiza wafanyabiashara kuona umuhimu wa maonyesho haya kwani yanatoa fursa nyingi za kiuchumi. Alieleza kuwa  kwa kuwa wafanyabiashara ni wengi ni vyema wanakatavi kujifunza ubunifu mpya kwa wengine ili kwa pamoja waweze kukua huku wakitangaza katavi kama sehemu ya utalii kwani kuna vivutio vingi ambavyo katika maonyesho hayo,

Kiongozi wa Chama pia alitoa nasaha zake akiwahimiza wananchi na wafanyabiashara kuendelea kutumia maonyesho haya kama jukwaa la kujitangaza na kuchangia ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Katavi na Tanzania kwa ujumla.

 Akihitimisha hotuba yake, Mkuu wa Mkoa alitoa rai kwa wananchi waliojiandikisha katika daftari la mkazi kuhakikisha wanajitokeza siku ya kupiga kura katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa tarehe 27/11/2024. Aliwakumbusha juu ya maendeleo yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya sita. Alisema ni vyema kuchagua kiongozi bora atakayeendeleza mafanikio yaliyopo kwa kuwa ni maendeleo endelevu kama kauli mbiu ya wiki ya mwanakatavi inayosema ’’Katavi yetu,Chagua Viongozi Bora wa Serikali za Mitaa, Imarisha Uchumi kwa Maendeleo Endelevu’’

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa