Pichani;Mtendaji wa Kata ya Katumba Bw.Revocatus Mapula mkutanoni akiwahamasisha Wananchi wa Kijjiji cha Mtambo kushiriki katika uchangiaji nguvu kazi katika Ujenzi wa madarasa katika Shule shikizi zilizopokea Fedha za UVIKO 19
Na: John Mganga-IO
Wananchi wa Kijiji cha Mtambo kilichopo Kata ya Katumba Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wametakiwa kujitoa kwa hali na mali kushiriki kikamilifu kuchangia nguvu kazi katika Ujenzi wa Vyumba vya madarasa ili kuunga mkono jitihada za Serikali kuboresha Miundombinu ya Elimu.
Shilingi Milioni Mia Moja Arobaini zinatarajia kutumika kwa ajili ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa 7 katika Shule shikizi pamoja na utengenezaji wa madawati katika Kijiji cha Mtambo kilichopo Kata ya Katumba Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo.
Fedha hizo zimetokana na Mgao wa Shilingi Bil 2.55 zilizotolewa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo na Serikali kwa ajili ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo kwa ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya Ugonjwa wa UVIKO 19.
Mtendaji wa Kata ya Katumba Bw.Revocatus Mapula amewaambia Wananchi wa Kijijij cha Mtambo kuwa Serikali imetoa fedha hizo kwa ajili ya Ujenzi wa Vyumba 7 vya madarasa katika Shule Shikizi ikiwa ni utekelezaji wa azma yake kuondoa kabisa changamoto ya Wanafunzi wanaosoma mbali na nyumbani.
Mpanda to Tabora road
Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda
Simu : 025 295 5164
Simu: 025 295 5164
Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz
Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa