• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Mwaka Mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan,Zaidi ya Bilioni 6 zaelekezwa Nsimbo,DC Mpanda,Mkurugenzi Nsimbo waeleza Mafanikio ya Serikali.

Imewekwa: March 19th, 2022

Pichani:Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh.Jamila Yusuph Kimaro akizungumza katika Mkutono wa Hadhara kueleza mafanikio ya Mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan katika eneo la Dipacha Kijiji cha Ndui Stesheni Kata ya Katumba  18 Machi 2022.


Nsimbo- Katumba

Katika Kipindi cha Mwaka mmoja wa Utawala wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo imepata mafanikio makubwa na ya kihistoria katika sekta mbalimbali Viongozi wa Wilaya wameeleza.

Kwa nyakati tofauti 18 Machi 2022 Mh.Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh.Jamila Yusuph Kimaro alipozungumza na Wananchi wa Kata za Sitalike Kijijini Magula  na Katumba Kijjini Ndui Stesheni  amewaambia Wananchi   kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja wa Utawala wa Mh.Rais Samia Suluhu Hassan, Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo imepata mafanikio makubwa kuwahi kutokea katika hitoria ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo.

DC Jamila amewaambia Wananchi wa Kata ya Katumba Nsimbo katika mkutano wa hadhara   kuwa katika kipindi cha Mwaka mmoja ukiacha Halmashauri nyingine Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo peke yake imepokea zaidi ya Shilingi Bilioni 6.

Ameeleza kuwa Fedha hizo zimeelekezwa kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Ujenzi wa miundombinu ya Elimu kama vile Vyumba vya Madarasa,Ujenzi wa Vituo vya Afya na Zahanati,pamoja na uboreshaji wa utoaji wa huduma kwa Wananchi.

 Kwa Upande wa Mapato ya ndani Mh Jamila pia amewaeleza Wananchi kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo hadi kufikia Februari imefanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Milioni 800 za mapato ya ndani ambapo Asilimia 40 ya makusanya hayo ya mapato ya ndani zimeelekezwa kutekeleza shughuli mbalimbali za miradi ya maendeleo.

Aidha DC Jamila ameeleza kuwa Mh.Rais Samia alielekeza na kuhimiza utengaji wa Asilimia 10 kwa ajili ya kuwawezesha akina mama,Vijana na  Watu wenye ulemavu kwa ajili ya kuwawezesha kujikwamua kiuchumi lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa Fedha zilizokusanywa kama ushuru kwa wananchi zinarudi kwa Wananchi hao kuteleleza miradi mbalimbali ambapo hadi kufikia Mwezi Februari Halmashauri imeendelea kutumia fedha za Asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kuwawezesha wau wa makundi hayo maalumu.

Kutokana na Mafanikio hayo yaliyopatikana katika kipindi cha awamu ya sita ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo  Mkuu huyo wa Wilaya alitoa rai kwa Wananchi kumuunga mkono Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan  kwa kuhakikisha kuwa wanashiriki kikamilifu katika  kuchangia nguvu kazi katika miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa.

DC Jamila ametoa rai kwa Wananchi  kulinda miradi mbalimbali iliyoanzizhwa na kutekelezwa na Serikali  ili kusudi ilete manufaa yaliyokusudiwa na Wananchi waweze kunufaika vema na miradi hiyo huku akiwasihi Wananchi kudumisha Amani na utulivu.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bi Tabia Nzowa kwanyakati tofauti alizungumza na Vyombo vya Habari kueleza Mafanikio ya Mwaka mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan alitumia fursa hiyo kumshukuru Rais Samia.

Bi Tabia alipozungumza na Shirika la Utangazaji Tanzania TBC Mkoa Wa Katavi wakati wa ziara yake kutembelea miradi iliyotekelezwa na Rais Samia kwa kipindi cha Mwaka mmoja ikiwa ni maandalizi ya Makala ya utekelzaji wa miradi hiyo alieleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo imepata bahati kubwa ya kupokea fedha nyingi zaidi kuwahi kutokea katika historia ya Halmashauri hiyo.

Kaimu Mkurugenzi Tabia  amemshukuru na kumpongeza Rais Samia  Suluhu Hassan kwa kazi kubwa aliyoifanya kwa kipindi cha Mwaka mmoja tangu aingie madarakani huku akiahidi kwa niaba ya Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo kusimamia vema utekelezaji wa miradi ya Serikali ili kuhakikisha kuwa  miradi inayoendelea kujengwa inakamilika kwa wakati,viwango  na kwa muda uliopangwa.

Kwa upande wao Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo pia wamemshukuru Rais Samia huku wakimtakia mafanikio mema katika utekelezaji wa majukumu yake mazito ya kuliongoza Taifa la Tanzania.

Mh.Rais Samia aliapishwa Rasmi 19 Machi 2021 kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Dkt John Pombe Magufuli aliyefariki Dunia 17 Machi 2021.

Pichani:Wananchi wa Kata ya Katumba wakimsikiliza aMkuu wa Wilaya ya Mpanda Mh.Jamila Kimaro wakati wa Mkutano wa hadhara wa kueleza mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa