• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

WASIMAMIZI WA VITUO NA WASIMIZI WASAIDIZI KATIKA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANOLEWA

Imewekwa: October 26th, 2025

Kuelekea uchaguzi mkuu unatarajia kufanyika Oktoba 29, 2025, wasimamizi wa vituo na wasimamizi wasaidizi katika vituo vya kupigia kura katika Jimbo la Nsimbo Mkoani Katavi wamepewa mafunzo elekezi ili kutekeleza majukumu yao kwa weledi.

Mafunzo hayo ya siku mbili yanayofanyika katika ukumbi wa shule ya Sekondari Nsimbo iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo yamefunguliwa leo na Msimamizi wa Uchaguzi katika Jimbo la Nsimbo Bwana Julius Zakaria Moshi ambapo amewataka washiriki wote katika semina hiyo kufuata sheria, kanuni, taratibu na miongozo inayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Bwana Moshi amewakumbusha wasimamizi hao pamoja na wasimamizi wasaidizi katika vituo vya kupigia kura kufuatilia kwa umakini mafunzo yanayotolewa nawatendaji wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili wawe watendaji wazuri na waendelee kuwa wazalendo, waaminifu na kufanya kazi kwa uadilifu kwa kufuata viapo vyao kwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Aidha, Bwana Julius Moshi amewataka wasimamizi na wasimamizi wasaidizi katika vituo vyao kuepuka kuwa chanzo cha migogoro na vyama vya siasa kwa kuvishirikisha vyama hivyo kupitia mawakala wa vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili na vinavyoshiriki uchaguzi mkuu katika hatua zote kwa kuzingatia matakwa, sheria, kanuni na maelekezo mbalimbali ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi.

Sambamba na hayo, Bwana Moshi amewataka wasimamizi na wasimamizi wasaidizi hao kusoma kwa makini Katiba, sheria, kanuni, miongozo na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na yanayotolewa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili kama kuna jambo lolote litawatatiza waweze kuuliza kwa watu sahihi na hatimaye kupata ufafanuzi wa jambo litakaloonekana kuwa na changamoto katika utekelezaji wa majukumu waliyopewa.

Kabla ya kufunguliwa kwa mafunzo hayo, Wasimamizi na wasimaizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Kata wamekula kiapo cha kutunza siri na kujivua uanachama kwa waliokuwa wanachama wa vyama vya siasa kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na madiwani mwaka huu.

Katika Jimbo la Nsimbo jumla ya wapiga kura 108,819 wanatarajia kupiga katika vituo 281 vya kupigia kura.

Itakumbukwa kwamba, Tuma Huru ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza Siku ya Jumatano ya taerehe 29/10/2025 kuwa siku ya Uchaguzi mkuu, ambapo watanzania wenye sifa watatumia haki yao ya kikatiba ya kumchagua Rais, wabunge na madiwani watakaowaongoza kwa kipindi cha miaka mitano.

KURA YAKO HAKI YAKO, JITOKEZE KUPIGA KURA

Matangazo

  • TANGAZO LA KUTEULIWA MAKARANI NA WATENDAJI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA NA KUITWA KUHUDHURIA MAFUNZO YA UCHAGUZI October 23, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA MRADI WA KITUO CHA AFYA IBINDI August 26, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WASIMAMIZI WA VITUO NA WASIMIZI WASAIDIZI KATIKA VITUO VYA KUPIGIA KURA WANOLEWA

    October 26, 2025
  • MAKARANI WAONGOZA WAPIGA KURA WAPEWA MAFUNZO - NSIMBO

    October 25, 2025
  • MADAKTARI WA SAMIA - TUMAINI JIPYA LA AFYA KWA WANANCHI WA NSIMBO

    September 30, 2025
  • “MADAKTARI WA SAMIA” WATUA NSIMBO, MKURUGENZI AWAKARIBISHA WANANCHI KUCHUNGUZA AFYA ZAO

    September 27, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa