• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Waziri Mkuu Mh.Kasim Majaliwa awakumbuka Yatima Nsimbo.

Imewekwa: November 10th, 2021

Pichani:Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh.Mwanamvua Hoza Mrindoko(Katikati) akikabidhi Zawadi mbalimbali kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kasim Majaliwa kwa Uongozi wa Kituo cha Gethsemane kilichopo Kata ya Litapunga Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo 10 Novemba 2021.


Na:John Mganga-IO Nsimbo DC

Mkuu wa Mkoa wa Katavi  Mh.Mwanamvua  Mrindoko amekabidhi zawadi mbalimbali kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kasim Majaliwa  kwa kituo cha kulelea watoto Yatima na waishio katika mazingira magumu cha Gethsemane kilichopo katika Kata ya Litapunga Halamashauri ya Wilaya ya Nsimbo.

Zawadi zilizokabidhiwa kwa Yatima na waishio katika Mazingira Magumu Gethsemane Nsimbo ni pamoja na Ngombe mmoja,Kilo 120 za Mchele, Lita 20 za Mafuta ya kupikia, Boksi mbili kubwa za Biskuti,pamoja na Pakti nane za Pipi.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya Zawadi hizo kwa Viongozi wa Kituo Hicho cha Gethsemane Mh.Mwanamvua amesema  Mh.Waziri Mkuu Kasim Majaliwa ametoa zawadi hizo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa  kufuatia  kuguswa na kutambua uwepo wa watoto Yatima na waishio katika Mazingira magumu katika Kituo hicho.

Mh.Mwanamvua licha ya pongezi kwa Shirika la Upendo na Sadaka linalosimamia Yatima na Waishio katika Mazingira Magumu Gethsemane, amewataka Viongozi wa Shirika hilo kufanikisha maono mazuri waliyonayo ya Uanzishaji wa Kituo cha Kulea watoto Yatima na Waishio katika Mazingira Magumu   kwa kuhakikisha kuwa Sheria,Miongozo na Kanuni mbalimbali za uanzishaji na  uendeshaji wa Vituo vya kulelea Yatima na waishio katika Mazingira magumu  zinazingatiwa.

Amesisitiza kuwa Lengo la Serikali kuweka Sheria,Kanuni na Miongozo mbalimbali inayosimamia uanzishwaji na uendeshwaji wa vituo hivyo ni kuhakikisha kuwa Watoto wanaolelewa katika Vituo hivyo wanalelewa kwa kuzingatia Utaratibu.

Aidha Mh.Mwanamvua amesema  ni muhimu Kituo hicho kuwajenga watoto katika misingi ya Maadili  ya  Kiroho  kusudi watoto hao wakue katika Misingi ya kumjua Mwenyezi Mungu na kwamba endapo jambo hilo litatiliwa mkazo Taifa litakuwa na hazina ya Raia wenye  Hofu ya Mungu jambo litakalopunguza na kuondoa kabisa changamoto ya mmomonyoko wa Maadili ya Taifa.

Katika Taarifa yake Mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi Kiongozi wa Mlezi ya watoto Kituoni hapo licha ya jitihada mbalimbali wanazochukua  amezitaja changamoto mbalimbali zinazowakabili kuwa ni  ukosefu wa Mabweni pamoja na Changamoto ya Mawasiliano kituoni hapo .

Regina Marius, mmoja wa watoto waishio Kituoni hapo akitoa shukrani  kwa niaba ya Watoto wenzake amemshukuru Waziri Mkuu Kasim Majaliwa na kusema kuwa daima watamkumbuka katika maombi kusudi Mwenyezi Mungu amjalie mafanikio katika Safari yake ya uongozi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Shirika hilo,Mwenyekiti wa Kamati ya Shirika hilo Sister Bernadetha Kihumbi amemshukuru Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Kasim Majaliwa kwa msaadaa alioutoa Kituoni hapo na kuahidi kumuombea kwa Mungu ili kusudi azidishiwe pale alipopunguza kusaidia watoto wa Kituo hicho.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa