• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Nsimbo District Council
Nsimbo District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa ndani
      • Habari ,Mawasiliano,TEHAMA na uhusiano
      • ununuzi na ugavi
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango,Takwimu na ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji na Udhibiti wa maji taka
      • Kilimo,umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Ujenzi
      • Mazingira na udhibiti wa taka ngumu
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
  • Fursa za uwekezaji
  • Huduma zetu
    • Elimu Msingi
  • Madiwani
    • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za shuguli za ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi mbalimbali
    • Maktaba ya picha
    • Jarida Mtandao la wiki la Halmashauri

Urasimishaji Ardhi wafanyika Kijiji cha Kasisi Nsimbo, Wakazi kupatiwa hatimiliki za Kimila bure.

Imewekwa: September 16th, 2021

Pichani:Afisa Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Damas Ngassa(Katikati) akitoa maelekezo wakati wa zoezi la Upimaji wa mashamba katika Kijiji cha Kasisi kabla ya Wapima Wasaidizi na Wasimamizi kuingia katika mashamba na maeneo ya Wananchi kwa shughuli ya Upimaji.

Zoezi la Urasimishaji mashamba na makazi kwa ajili ya utoaji wa hatimiliki za Kimila Katika Kijiji cha Kasisi kinachotekeleza Mpango wa matumizi bora ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo limekamilika kwa mafanikio makubwa Afisa Ardhi Nsimbo Bw.Damas Ngassa ameeleza.

Idadi kubwa ya Wananchi katika Kjiji cha Kasisi wamejitokeza kurasimisha Maeneo ya makazi pamoja na Mashamba kufuatia Elimu na Hamasa iliyotolewa kwa makundi mbalimbali kuhusu faida za Urasimishaji Ardhi pamoja na umuhimu wa hatimiliki za Kimila ambapo zaidi ya hatimiliki za Kimila 3000 zinatarajiwa kuandaliwa na  kutolewa bure kwa Wananchi wa Kijiji cha  Kasisi waliojitokeza kurasimisha maeneo yao.

Zoezi hilo lililodumu kwa takribani siku 30 limehusisha Vitongoji Vinne vya Kijiji cha kasisi ambavyo ni Iseka,Kasisi,Iyogelo na Mabiti likifadhiliwa na Taasisi ya JGI(Jane Goodal Istitute)chini ya Mradi wa LCWT(Landscape Conservation in Wester Tanzania) ambapo Wananchi katika maeneo hayo wamepimiwa maeneo yao bure na mara baada ya taratibu za uhakiki na uandaaji  kukamilika Wananchi hao watapatiwa Hatimiliki bure bila malipo yoyote.

Afisa Ardhi Nsimbo Bw.Damas Ngassa ameeleza  kuwa zoezi la Urasimishaji maeneo ya makazi pamoja na mashamba katika Kijiji cha Kasisi limefanyika kwa kuwahusisha Wataalamu wa Ardhi kutoka Ofisi ya Ardhi Nsimbo, Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Mkoa pamoja na baadhi ya  Wananchi ambao walitoka katika Kijiji cha Kasisi ambapo Taasisi ya JGI pia ilifadhili  Mafunzo ya kuwajengea uwezo  Wananchi hao  ili waweze kushiriki  utekelezaji wa  zoezi hilo kama Wapima Wasaidizi wakishirikiana na Wajumbe wa Kamati ya ardhi ya Kijiji kama Wahakiki kwa kutumia Teknolojia ya Vishkwambi.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU February 25, 2025
  • MICHORO YA RAMANI KWA ZABUNI ZILIZOTANGAZWA KATIKA SHULE MBALIMBALI September 16, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 20, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 01, 2024
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WANANCHI NSIMBO WATAKIWA KUJITOKEZA KUBORESHA TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA MPIGA KURA

    May 01, 2025
  • WAFANYAKAZI WAPEWE MOTISHA KAZINI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI NSIMBO LARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

    April 30, 2025
  • KAMISHNA WA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI ATEMBELEA MAFUNZO YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI NA WAENDESHA VIFAA VYA KIELEKTRONIKI VYA BAYOMETRIKI (BVR KITS) KATIKA JIMBO LA NSIMBO

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Video zaidi

Quick Links

  • Mfumo wa Tausi Portal
  • Watumishi Portal
  • Wezesha Portal
  • Mfumo wa FFARS
  • Mfumo wa PLANREP
  • Mfumo wa SIS
  • Kupata matokeo ya kidato cha nne ingia hapa

Kurasa zinazohusana

  • President's Office
  • Tanzania Government Portal
  • Public service Management
  • Public Service Recruitment
  • PO- RALG

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    Mpanda to Tabora road

    Anuani ya Posta: P.O.Box 688 Mpanda

    Simu : 025 295 5164

    Simu: 025 295 5164

    Barua pepe: ded@nsimbodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Malalamiko
    • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
    • Ramani
    • Huduma

Hatimiliki@2016GWF.Haki zote zimehifadhiwa